Uk. 4 Uk. 18 Uk. 14

Transcription

Uk. 4 Uk. 18 Uk. 14
Toleo NO. 039
Julai –Septemba 2011
Uk. 4
Bei Shs. 500/=
Uk. 14
Wakulima wapongeza MVIWATA kwa
kuhabarisha wakazi wa vijijini
ISSN 0856-5937
Uk. 18
Maonesho ya NaneNane 2011
Kijana mbunifu atengeneza mitambo ya radio
kunufaisha wanakijiji
Tahariri
Toleo NO. 039
Julai Septemba 2011
Bei Shs. 500/=
ISSN 0856-5937
WAHARIRI
Susuma Msikula Susuma
Stephen Ruvuga
BODI YA MVIWATA
Mwenyekiti – Yazid Makame
Makamu Mwenyekiti – Lydia Ruliho
Katibu - Stephen Ruvuga- (Mkurugenzi Mtendaji)
Mweka Hazina - Grace Runkulatile
I
WAJUMBE
Cosma Bulu
Sylvester Yatuba
Joseph Kilowoko
Samweli Maseke
Julius Mbago
Habibu Simbamkuti
MSHAURI WA MVIWATA
Prof. Amon Mattee
LINATOLEWA NA
KUSAMBAZWA NA
Mtandao wa Vikundi vya
Wakulima Tanzania (MVIWATA)
S.L.P 3220 Morogoro, Tanzania
Simu:023 261 41 84
Faksi:023 261 41 84
Barua pepe: [email protected],
[email protected]
Tovuti: www.mviwata.org
MICHORO
Godwin Chipenya
USANIFU NA
UCHAPISHAJI
PENplus Ltd – 022 2182059
Toleo NO. 039
Julai –Septemba 2011
Uk. 4
Bei Shs. 500/=
Uk. 14
Wakulima wapongeza MVIWATA kwa
kuhabarisha wakazi wa vijijini
ISSN 0856-5937
Habari za vijijini zipewe
kipaumbele
ngawa juhudi na mchango wa jamii za vijijini nchini Tanzania
ndiyo vinavyoiendeleza Taifa, habari za vijijini haziandikwi kwa
umuhimu huo.
Mara nyingi, habari za vijijini zinazopewa nafasi kwenye
vyombo vya habari ni zinazohusu maafa, kesi, vimbwanga na hotuba
za viongozi wanapotembelea maeneo hayo.
Wanahabari wanafanya kazi kubwa ya kuuelimisha umma, hata
hivyo kwa sehemu kubwa habari hizo zimekuwa ni zile zinazohusu
watu wa mijini.
Toleo hili linalozungumzia habari za vijijini ni sehemu ya
utekelezaji wa ajenda ya upashanaji habari inayotekelezwa na
MVIWATA kwa muda mrefu sasa.
Tunafahamu kwamba pamoja haya umuhimu wa upatikanaji wa
habari kwa watu wa vijijini, ziko changamoto kadhaa zinazokwamisha
ufanisi wake.
Miongoni mwa changamoto hizo ni ukosefu wa vitendea
kazi ikiwemo usafiri, kamera na vinasa sauti ambapo hata
waandishi wachache wenye nia ya kwenda kukusanya habari vijijini
wameshindwa kufanya hivyo kwa kukosa usafiri na wengine kuishia
kutegemea usafiri wa viongozi wanapotembelea maeneo ya vijijini.
Kulingana na kubanwa na ratiba za viongozi hao, waandishi hawawezi
kukusanya habari nzuri zenye kuchochea maendeleo ya vijijini zaidi
ya kuishia kuandika hotuba na maagizo ya viongozi.
Changamoto nyingine ni ya waandishi wa habari kukosa
taaluma ya kutosha yenye kuwawezesha kudadisi na kuibua kero na
changamoto halisia za vijijini na siyo vimbwanga.
Tunaamini ziko changamoto nyingi na lengo letu siyo kuziainisha
zote isipokuwa tunawakumbusha wadau wa sekta ya habari kuwa
vijijini ndiko kwenye chimbuko la wazalishaji na kwamba hatupaswi
kuwatenga.
Tunashauri kuwepo na jitihada za makusudi za kutatua
changamoto hizi na vilevile kuwe na juhudi za kuhimiza vyombo
vya habari kuzipa kipaumbele habari za vijijini. Ni wakati muafaka
ambapo
Tunawakumbusha wana habari juu ya umuhimu wa kuzingatia
maadili ya taaluma ya uandishi wa habari kwa kuandika habari
zilizofanyiwa utafiti wa kina na kuhakikisha jamii zote vijijini na
mijini wananufaika na huduma hii muhimu.
Tusaidie kuchochea maendeleo vijijini kwa kuhakikisha
tunawapatia habari za kutosha na zilizofanyiwa utafiti.
Uk. 18
Maonesho ya NaneNane 2011
Kijana mbunifu atengeneza mitambo ya radio
kunufaisha wanakijiji
Picha ya Jalada:
Bw. Benjamini Nziku mkulima wa
kijiji cha Lusala kata ya Lupanga
wilayani Ludewa akipata habari
kupitia gazeti la wakulima la
Pambazuko.
b
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
MADA MAALUM
Upatikanaji wa habari vijijini,
kichocheo cha maendeleo?
teknolojia ya habari, nchi za Kusini
mwa Afrika bado zinakabiliwa na
tatizo kubwa la kukosekana kwa
habari za umma hasa kwenye maeneo
ya vijijini ambazo ni muhimu kwa
wananchi kutoa maamuzi mbalimbali
ambayo ni sahihi kwa maisha yao.
maeneo hasa ya vijijini. Mfumo wa
upashanaji habari uliopo sasa siyo
utokana na kupiga hatua
wa kuridhisha kwani haumfikii kila
mwananchi wa kijijini mahali alipo.
za kimaendeleo katika
Kwa mfano magazeti yanayofika
teknolojia hasa ya habari,
kwa
nadra
vijijini ndani yake yanakuwa
wigo wa upatikanaji wa habari
yamejaa
habari
zinazohusu vuguvugu
hivi sasa umepanuka ukilinganisha
la maisha ya mjini. Habari hizo nyingi
na miaka ya nyuma hasa wakati
Hata
ni zile zinazohusu malumbano na
tunapata uhuru.
siasa za chuki baina ya viongozi
radio za kijamii
Hivi sasa watu wanauwezo
wa vyama, foleni za barabarani,
wa kutumia kompyuta na
zilizoanzishwa kwa lengo
michezo ambayo pengine mtu
simu za mkononi zenye
kijijini hajawahi kuiona na
la kuhudumia wakazi wa vijijini, wa
huduma ya intaneti na
burudani kama vile miziki
kuweza kupata taarifa
zimeacha misingi ya kuanzishwa na picha kubwa kubwa za
mbalimbali
zinazotokea
wasanii ambazo ki uhalisia
kwake na kuegemea zaidi
ulimwenguni kwa wakati
hazimuongezei tija mtu wa
huo huo ama kulipia huduma
kutangaza mambo ya
kijijini katika harakati zake za
mbalimbali kama vile matibabu,
kupambana na umasikini kupitia
mijini.
maji na umeme. Lakini pia wanaweza
kilimo, ufugaji ama uvuvi.
hata kufanya manunuzi ya bidhaa
Bado
Tunashuhudia ongezeko la
mbalimbali kupitia intaneti na hivyo kuna changamoto zinazoikumba vyombo vya habari vya kielektroniki
kupunguza gharama na muda na sekta hii ya habari ikiwemo uhaba kama vile radio na televisheni na
kurahisisha biashara.
wa upatikanaji wa habari sahihi ukuaji wake kutoka kwenye mfumo
Hata hivyo mbali na kukua kwa na zenye manufaa kwa baadhi ya
Endelea Uk wa 2
Na Goodness Mrema, Morogoro
K
Mwekahazina wa MVIWATA Ruvuma Bibi Immaculata John akitekeleza shughuli za MVIWATA za kusambaza habari za wakulima kwa
wadau
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
1
MADA MAALUM
Upatikanaji wa habari vijijini
Inatoka uk. wa 1
wa analogia kwenda digitali.
Ongezeko na ukuaji wa
teknolojia bado hauwanufaishi
vya kutosha wakazi wa vijijini.
Kilichobadilika ni kuwepo kwa
usikivu mzuri wa matangazo ya
radio kwenye baadhi ya vijiji tofauti
na ilivyokuwa awali. Habari zenye
mlengo wa kuchochea maendeleo
vijijini bado hazipewi kipaumbele.
Hata
radio
za
kijamii
zilizoanzishwa kwa lengo la
kuhudumia wakazi wa vijijini,
zimeacha misingi ya kuanzishwa
kwake na kuegemea zaidi kutangaza
mambo ya mijini.
Japokuwa televisheni na redio
zinajitahidi kurusha matangazo
yake na kuwafikia kwa wakati watu
wa vijijini, lakini bado habari zake
zinakosa mguso kwao, ingawa serikali
inajinadi kuwa matumizi ya mfumo
wa digitali yameongeza upatikanaji
wa habari maeneo ya vijijini.
Kwa ujumla habari zinazohusu
mafundisho ama mafanikio ya
wananchi vijijini haziandikwi wala
kusikika vya kutosha na kwamba
kuna haja ya kubadili mfumo
ili waandishi wa habari wapate
msukumo wa kuwafikia wananchi
vijijini na kuandika habari zao.
Siku hizi umekuja utaratibu
mpya wa upashanaji habari kupitia
mitandao mbalimbali ya kijamii
(tovuti, blogs, facebook, twitter)
ambayo kwa hakika mkulima au
mfugaji mdogo anayeishi kijijini
hafahamu hata jinsi ya kuitumia na
wachache wenye uelewa hawawezi
kuitumia kwa kukosa nishati ya
umeme.
Changamoto ya
miundombinu
Ziko sababu nyingi zinazotajwa
kuchangia habari kutowafikia watu
wa vijijini. Sababu mojawapo ni ubovu
wa miundombinu ya barabara katika
maeneo mengi ya vijijini ambako
kuna asilimia 80 ya Watanzania
wazalishaji wanaochangia pato la
taifa.
Kulingana na miundombinu
duni ya barabara zetu hasa maeneo
2
ya vijijini, ni vigumu kwa mwananchi
wa kijijini kupata gazeti kwa wakati
na kulisoma.
Wauzaji na wasambazaji wa
magazeti ya kila siku wanajikuta
wakishindwa kuyafikia maeneo hayo
kwa wakati. Kwa mfano gazeti la
kila siku linalosambazwa asubuhi
katika maeneo ya mijini huchukua
wakati mwingine siku mbili kufika
eneo la Mrimba Kilombero mkoani
Morogoro kutokana na barabara ya
kuelekea sehemu hiyo kuwa mbaya.
Huu ni mfano wa sehemu moja
iliyo katika mkoa jirani na mji ambapo
magazeti mengi huchapishiwa, swali
ni je vipi kwa watu waishio Kigoma
vijijini, Karagwe ama Murugwanza
huko Ngara, wao hulipata gazeti hilo
siku ngapi baada ya kuchapishwa?
Ukosefu wa nishati nalo ni tatizo
kubwa kwa wakazi wa maeneo ya
vijijini ambalo linazuia wananchi
wa vijijini kununua televisheni
au radio kwa sababu ya kukosa
nishati itakayowawezesha kuvitumia
vyombo hivyo.
Maisha magumu ya vijijini
yanayosababishwa na ukosefu wa
huduma muhimu za kijamii pia
yanadhoofisha kasi ya upatikanaji
wa habari vijijini. Kwa mfano
mtu anayesumbuliwa
na maradhi kwa
kukosa huduma
sahihi
za
matibabu,
hawezi kukaa
na kusikiliza
radio
huku
akigugumia
kwa maumivu
makali. Mtu huyu
pia hawezi kutenga
fedha ya kununua gazeti
linalomfikia baada ya siku mbili
Akina mama wengi vijijini
wanakosa muda wa kusikiliza taarifa
za habari ama matangazo mengine
muhimu kwa kuwa muda ambao
radio na televisheni zinatangaza
taarifa za habari wao wanakuwa
kwenye shughuli za kupika, kutafuta
maji na kuni na shughuli za shamba.
Ukiachana
na
tatizo
la
miundombinu duni, iko sababu
nyingine ya baadhi ya wananchi kukosa
mwamko wa kutafuta ama kutoa
habari. Wananchi kwenye baadhi ya
maeneo ya vijijini hawajaelimishwa
vya kutosha juu ya umuhimu wa
kutoa na kupokea habari kuhusiana
na masuala mbalimbali hivyo baadhi
yao kuona kwamba kununua gazeti
ama kununua televisheni ni kuwa na
matumizi ya anasa.
Habari zinachochea
maendeleo?
Wakazi wa vijijini wengi wao wakiwa
ni wakulima waliopata fursa ya
kuzungumzia hoja hii, walikiri kuwa
upatikanaji wa habari sahihi vijijini
umesaidia kuchochea maendeleo,
japokuwa kiwango cha upatikanaji
wake siyo cha kuridhisha.
Walieleza kuwa habari chache
zilizowafikia ziliwasaidia kupata
elimu ya kilimo bora, taarifa za
upatikanaji wa pembejeo, masoko,
mwelekeo wa hali ya hewa na
mwenendo wa uchumi na hali ya
kisiasa nchini pamoja na kufahamu
jitihada za maendeleo zinazofanywa
na makundi mbalimbali.
Mbali na
vyombo vya habari,
ziko njia nyingine za asili
zinazotumika kufikisha habari kwa
jamii kwenye maeneo ya vijijini ikiwemo
mikutano ya vijiji, kwenye nyumba
za ibada na kwenye mikusanyiko
kama vile sokoni na kwenye
minada.
Walisema habari hizo pia
zinawapatia uwanja mpana wa
mjadala na kubadilishana uzoefu
kuhusiana na masuala mbalimbali
yanayowakabili ikiwemo uwezo wa
kudai haki zao za msingi.Wanafahamu
mahali pa kupata mahitaji muhimu na
fursa zinazopatikana kwa ajili yao na
Endelea Uk wa 3
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
MADA MAALUM
Inatoka uk. wa 2
njia muafaka za kufikia suluhu kwa
changamoto zinazowakabili katika
shughuli zao.
“Suala la upatikanaji wa habari
linahusika zaidi na maisha ya kila
siku ya mwananchi. Ni suala la
maendeleo ya kila mwanadamu hapa
ulimwenguni, endapo wananchi hawa
wa vijijini watapata habari sahihi na
kwa wakati zitachochea bidii katika
kujiletea maendeleo,” alisema Bw
Andrew Hepelwa, Katibu Mkuu
Mstaafu wa MVIWATA taifa.
Aliongeza kuwa maendeleo
ni jambo la muhimu ambalo kila
mwanadamu analitegemea katika
maisha yake kuanzia ngazi ya familia
hadi ngazi za kitaifa. Kama hupati
taarifa kamili kuhusu kitu fulani,
huwezi kujua uzito wake na huwezi
kuchukua hatua za kimaendeleo na
kwa upande mwingine jamii ikipata
taarifa na habari sahihi inaweza
kuchukua hatua ya kujikwamua
katika matatizo.
Matumizi ya habari
Kwa ujumla jamii ya vijijini kutokana
na kutengwa kwa muda mrefu na
mfumo wa habari, nayo kwa namna
fulani imekuwa kama imejiengua na
kuyaona masuala ya habari kama
siyo sehemu yao.
Jamii hii inahitaji kujengewa
ufahamu wa kutosha kuhusu
umuhimu wa kupashana habari
na matumizi sahihi ya vyombo vya
habari katika kujiletea maendeleo.
Vyombo vya habari katika hili vina
mchango mkubwa wa kuwafumbua
macho wakazi wa kijijini ili wafahamu
umuhimu wa matumizi sahihi ya
habari katika mchakato wa kujiletea
maendeleo.
Mbali na vyombo vya habari, ziko
njia nyingine za asili zinazotumika
kufikisha habari kwa jamii kwenye
maeneo ya vijijini ikiwemo mikutano
ya vijiji, kwenye nyumba za ibada
na kwenye mikusanyiko kama vile
sokoni na kwenye minada.
Hata hivyo taarifa nyingi muhimu
hutolewa katika mikutano ya vijiji,
lakini kutokana na kukosa mwamko
huko nako mahudhurio ni madogo
na hivyo kukosesha wananchi habari
muhimu.
Miongoni
mwa
wakulima
waliohojiwa wamekiri wazi kuwa
hawajawahi kuhudhuria mkutano
wa kijiji kwa zaidi ya miaka miwili.
Hili ni tatizo na ni tabia inayopaswa
kuachwa kwa sababu inadidimiza
maendeleo.
Miongoni mwa wakulima hao
pia wamekiri mapungufu kwamba
walipata habari lakini hawakuzitumia
ipasavyo jambo ambalo wamelijutia
na baadaye kujirekebisha. Kwa
mfano Bw. Charles Ndugulile
mkulima wa kijiji cha Mwamala Kata
ya Mwamala wilaya ya Shinyanga
Vijijini alisema “mwaka 2008 kupitia
matangazo ya radio nilipata taarifa za
kutokea mabadiliko ya tabia ambayo
yatasababisha ukame na mlipuko wa
wadudu lakini nilipuuzia na baadaye
msimu wa kilimo uliofuata nililima
shamba kubwa kama kawaida,
nikapata hasara baada ya mazao
kukauka kwa ukame.”
Bw.
Ndugulile
akafafanua
kwamba kutokana na hali hiyo
amekuwa mhamasishaji mkubwa
kwenye mkoa wa Shinyanga
akiwahimiza wakulima umuhimu
wa kutafuta habari na kuzitumia,
lakini pia wawe wamezipata kutoka
katika vyanzo vya uhakika na
vinavyoaminika ila wasipotoshwe
kwa kupata habari ambazo si sahihi.
Hitimisho
Ili kuboresha upatikanaji wa habari
vijijini, serikali na wadau wa habari
kwa ujumla wanapaswa kushirikiana
kuondoa kasoro zilizopo na kuweka
mfumo wa usawa wa utoaji taarifa
na upatikanaji wa habari kwenye
Endelea Uk wa 5
Upatikanaji wa habari sahihi unapanua wigo wa mijadala kama hii ya wakulima
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
3
MADA MAALUM
Maoni ya wakulima na
wataalam
Na Goodness Mrema
C
hangamoto
kubwa
inayowakabili
wakulima
vijijini kwa kukosa habari
ni kuachwa nyuma kimaendeleo,
kuibuka kwa migogoro mingi baina
yao na viongozi wao ama makundi
mengine katika jamii.
Baadhi ya wakulima na wataalam
wamekuwa na maoni tofauti
kuhusiana na suala hili la upatikanaji
wa habari vijijini. Wakulima kutoka
mikoa mbalimbali walieleza jinsi
wanavyokabiliwa na changamoto
katika kupokea na kutoa habari
katika maeneo mengi ya vijijini
kutokana na miundombinu mibovu.
Yafuatayo ni maoni waliyoyatoa
baada ya kuulizwa swali lililosema
hali ya upatikanaji wa habari kijijini
ukoje?
Bibi. Mariam Mmanga
kutoka kijiji cha Kivulini wilayani
Mwanga mkoani Kilimanjaro alieleza
kwamba japokuwa kijijini kwake
hawatembelewi na waandishi wa
habari mara kwa mara wala kufikiwa
na magazeti, lakini wanawake
kijijini kwake wamejiunga katika
vikundi wanavyovitumia kupashana
habari kupitia mikutano na vikao
mbalimbali na sasa wamehamasika
na wanaelewa umuhimu wa kupata
habari, jambo ambalo linawatia moyo
na wanaimani kwamba hawataweza
kubaki nyuma kwani wanafahamu na
wanaelewa nini kinaendelea katika
nchi yao. Hata hivyo akaongeza
kuwa wanaomba kutembelewa na
wanahaabari ili habari za vikundi
vyao pia zitangazwe.
Bibi.
Mariam
Hassan
kutoka kijiji cha Magamba, wilayani
Kibondo mkoani Kigoma anaeleza
kwamba magazeti kijijini Magamba
yanawafikia baada ya siku tatu ama
nne, tena lazima awepo mtu ametoka
mjini siku hiyo. Kwa upande wa radio
wanakamata zaidi radio za Burundi
na kwamba hupokea matangazo ya
radio moja tu ya Tanzania ambayo
nayo husikika usiku tu, jambo ambalo
linawafanya washindwe kupiga hatua
kimaendeleo.
Ameiomba serikali kuwakumbuka
Endelea Uk wa 5
Miongoni mwa machapisho yanayotolewa na MVIWATA ambayo yamewanufaisha wakulima wengi kwa kuwapata habari sahihi za kilimo
4
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
MADA MAALUM
Inatoka uk. wa 4
na kuhakikisha kwamba nao pia
wanapata huduma hii muhimu kwani
wanaonekana wamesahaulika kama
vile wako nje ya Tanzania kutokana
na kijiji chao kuwa mpakani mwa
nchi ya Burundi. “Kuhusu habari za
kijijini kwetu zinaandikwa pale tu
kiongozi anapokuja kututembelea
ama wakati mwingine waandishi
hufika kijijini hapo kunapokuwa
na matukio ya maafa kama vile
mauaji. Tatizo hili linatuathiri zaidi
sisi wanawake kwani muda mwingi
tuko ndani, afadhali wenzetu
wanaume wanakutana kwenye
vikao na kuhabarishana na wengine
wanamiliki simu za mkononi.”
Bw.
Hamad
Abdallah
Salimin kutoka Zanzibar yeye
alieleza kukerwa na waandishi wa
habari wanaokurupuka na kutangaza
mambo yasiyo sahihi na kuupotosha
umma. Akashauri
ni
vyema
wanataaluma hawa kuthibitisha
habari wanazozikusanya kabla ya
kuzitangaza kwa umma.
Hata hivyo aliwashauri wakulima
wenzake wakabiliane na changamoto
ya upatikanaji wa habari katika
maeneo ya vijijini kwa kutosubiri
tu hadi magazeti yawafikie ndipo
wajue wamepata habari kumili kujua
nini kinaendelea, bali wanaweza pia
kupata habari zinazowahusu kwa
kupitia majarida yanayochapishwa
na
mashirika
yanayojihusisha
na shughuli za kilimo kama vile
MVIWATA ili kutambua fursa walizo
nazo.
Lakini akasema kwamba wakulima
wasiishie kusoma habari na kuziacha
tu katika makaratasi bali wazifanyie
kazi na pia wasiogope kutumia
vyombo vya habari kuwasilisha kero
na kufichua maovu.
Bw. Joseph Msagama kutoka
Tanga alikiri kuwa changamoto
kubwa ipo katika upokeaji wa habari
kutokana na uhaba wa rasilimali
fedha ambayo inamwathiri kila
mkulima.
“Jambo la kusikitisha ni kwamba
wananchi wa vijijini wanaonekana
kuwa tabaka la watu waliosahaulika
katika kila kitu kuanzia kipato, elimu
na hata haki zao mbalimbali ikiwemo
hii ya kupata habari” alisema Bw.
Msagama.
Alishauri Halmashauri za wilaya
ziweke utaratibu wa kutenga
mafungu ya kuwawezesha usafiri
maaalum waandishi wa habari
ili wafike maeneo ya vijijini na
kuwasaidia wananchi kufahamu
nini kinaendelea na kwa kiasi gani
kinaathiri uchumi wa wakulima.
Kwa upande wake Bw. Abdala
Ramadhani kutoka wilaya ya
Misungwi, Mwanza alisema wakulima
wengi vijijini wanakabiliwa na uhaba
wa habari na kushauri vituo vya
taarifa vijijini viimarishwe ili kuziba
pengo lililopo.
“Kupitia vituo hivyo vichache
vilivyopo
sasa
wakulima
na
wajasiriamali
wanapata
habari
kuhusiana na bei za mazao na wapi
wanaweza kuuza lakini habari hizo
haziwafikii wengi kutokana na uhaba
wa rasilimali fedha unaozikabili,”
alisema Ramadhani.
“Tunashukuru kuwapo kwa
gazeti letu wakulima la Pambazuko,
linatuwezesha kufahamu wenzetu
katika maeneo mengine wanafanya
nini na ni njia gani wanazozitumia
kutatua changamoto zao, jambo
ambalo linatupa ari ya kufanya kazi
kwa bidii ili kuzalisha kwa tija.”
Bw. Ramadhani alisema kupitia
mtandao wa wakulima wanajipanga
ili kuweka utaratibu mzuri wa
kuwezesha habari za wakulima
wa Mwanza zinamfikia mhariri wa
Pambazuko kwa wakati.
Bw. Paul Mossama kutoka
Serengeti mkoani Mara, anaeleza
kuwa mfumo wa upashanaji habari
uliopo nchini hivi sasa ni mzuri
kuliko miaka ya nyuma, japokuwa una
kasoro ya kutotangaza habari nyingi
za kuwasaidia wakulima kuboresha
shughuli zao na akashauri vituo vya
radio na televisheni vinavyoanzishwa
na halmashauri za wilaya vitangaze
zaidi habari hizo badala ya kuwa na
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
Endelea Uk wa 6
Upatikanaji wa
habari vijijini
Inatoka uk. wa 3
maeneo ya vijijini na mijini.
Kwa upande wa radio
matangazo yaboreshwe yasikike
vizuri vijijini ili wananchi wetu
walioko mipakani kama vile
Kigoma pia waweze kunufaika
na matangazo ya radio za nchini
mwao badala ya radio za nchi jirani
ya Burundi na Kongo ambazo
kila kukicha zinatangaza vita na
mauaji kutokana na mapigano
yanayoendelea nchini mwao.
Kadhalika
waandishi
wenyewe
wanakabiliwa
na
changamoto ya kujiendeleza
kitaaluma ili kuweza kuwa
na upeo zaidi wa kuandika
na kuchanganua habari zao
kwa weledi hasa zinazohusu
maendeleo vijijini badala ya kuwa
mawakala ama mashabiki wa
siasa tu.
Kuna matatizo mengi vijijini
ambayo kimsingi yanahitaji nguvu
ya wanahabari kuyatatua. Kwa
mfano wanahabari wanapaswa
kuijengea uwezo jamii kuhusu
elimu ya afya vijijini, elimu ya
ukatili wa wanawake na vitendo
vya unyanyasaji, elimu juu ya
umiliki na matumizi bora ya ardhi,
elimu ya kilimo bora na ufugaji,
ujasiriamali, masoko na umuhimu
wa elimu kwa watoto wao.
Ipo haja kubwa ya tasnia
ya habari kutilia mkazo suala la
kuielimisha jamii ili iepukane na
imani potofu za kwenda kwa
waganga wa kienyeji kupiga ramli
badala ya kuwapeleka wagojwa
kutibiwa kwenye zahanati na
vituo vya afya.
Wanakijiji ambao kwa sehemu
kubwa ni wakulima wanapaswa
kujengewa uelewa wa masoko
ya mazao yao, taarifa za bei na
mbinu bora za kuongeza tija katika
uzalishaji na kuboresha uchumi.
Maendeleo
vijijini
yanachelewa
kwa
sababu
wananchi hawapati habari sahihi
kwa wakati muafaka. Hivyo
yanapaswa kuchochewa kwa
kuwapatia habari za kina.
5
MADA MAALUM
Maoni ya wakulima...
Inatoka uk. wa 5
vipindi vingi vya miziki na salamu.
Akashauri pia magazeti kutenga
kurasa maalumu zitakazoandika
habari za wakulima wadogo angalau
mara moja kwa wiki. “Magazeti
mengi sasa yamefungua kurasa za
udaku, urembo na muziki, hivyo hata
kwa habari za wakulima jambo hili
linawezekana.”
Aliwashauri wakulima wadogo
kutumia mitandao ya wakulima
waliyonayo katika maeneo yao
kwa ajili ya kupashana habari
hadi pale wanapokuwa wanaona
wameshindwa
kufanya
hivyo
wenyewe ndipo waweze kumtafuta
mwandishi ambaye atawasaidia
kutangaza taarifa zao ili nao
wapate nafasi ya kupaza sauti zao
na kusaidiwa pale wanapohitaji
msaada.
Bw. Benardi Maiko kutoka
Kasanga, wilayani Sumbawanga
mkoani Rukwa alisema wakulima
wanayo mambo mengi ambayo ni
vyema wakayatangaza ikiwemo
mazao yao na bidhaa zingine
wanazozalisha, changamoto ya uhaba
wa pembejeo na zana bora za kilimo
pamoja na mahitaji ya masoko ya
kuuzia mazao yao.
Aliongeza
pia,
wakulima
wanahitaji kuwezeshwa kuwasiliana
wao kwa wao kupitia vyombo vya
habari ili kurahisisha mawasiliano
kwani badala ya wao kufunga
safari kwenda maeneo mengine
kuwatembelea wenzao wataweza
kusoma tu kwenye magazeti ama
kusikiliza radioni na kujifunza.
“Endapo habari zingekuwa zinafika
maeneo ya vijijini kama ilivyo kwa
maeneo ya mijini hakika wakulima
leo tungekuwa kundi lenye nguvu
kiuchumi na tusingekandamizwa
wala kunyanyaswa” alisema Bw.
Maiko
Bw. Charles Ndugulile
mkulima wa kijiji cha Mwamala
Kata ya Mwamala wilaya ya
Shinyanga Vijijini alieleza kwamba
6
upatikanaji wa habari unategemeana
na watafutaji wa habari kwamba
wanataka habari za namna gani na
zinazohusu nini na kutolea mfano
wa jarida la Pambazuko kwamba kila
anayetaka kupata habari kuhusiana
na wakulima anaweza kuzipata
kutoka ndani ya jarida hilo.
Akizungumzia matumizi sahihi
ya habari Bw. Ndugulile alisema
“mwaka 2008 kupitia matangazo
ya radio nilipata taarifa za kutokea
mabadiliko ya tabia ambayo
yatasababisha ukame na mlipuko wa
wadudu lakini nilipuuzia na baadaye
msimu wa kilimo uliofuata nililima
shamba kubwa kama kawaida,
nikapata hasara baada ya mazao
kukauka kwa ukame.”
Bw. Ndugulile alifafanua kwamba
kutokana na hali hiyo amekuwa
mhamasishaji mkubwa kwenye katika
mkoa wa Shinyanga akiwahimiza
wakulima umuhimu wa kutafuta
habari na kuzitumia, lakini pia wawe
wamezipata kutoka katika vyanzo
vya uhakika na vinavyoaminika ila
wasipotoshwe kwa kupata habari
ambazo si sahihi.
Alifafanua kwamba katika mkoa
wa Shinyanga wamewahamasisha
wakulima umuhimu wa kutafuta
habari kutoka katika vyanzo vya
uhakika na vinavyoaminika ili
wasipotoshwe kwa kupata habari
ambazo si sahihi.
Alisema kuwa wakulima wanaumia
waonapo habari mara kwa mara
zinazoeleza kuwa wameshindwa
kufanya jambo ama wana mgogoro
fulani wakati habari za mafanikio
waliyopata kupitia kilimo ikiwemo
kuongeza uzalishaji na kuweza
kulipa ada za watoto wao, kujenga
nyumba, kuongeza idadi ya mifugo
na hata kufanikiwa kununua zana za
kilimo, haziandikwi. “Kwa msingi huu
ndiyo maana mara nyingi nimekuwa
nikishauri kwamba ni muhimu
wakulima
tuimarishe
chombo
chetu cha habari kama Pambazuko
kinachoweza kutusemea habari
zetu.”
Bw. Ndugulile ambaye pia
ni mwenyekiti wa MVIWATA
Shinyanga, alisema vyombo vingi
vya habari nchini hivi sasa vinafanya
shughuli zake kibiashara na hivyo
kujikita katika matukio yenye
habari zinazouzika na kutupa kando
jukumu la kuwaelimisha wakulima
kilimo biashara ama ufugaji na uvuvi
wa kisasa.
Maoni ya wataalam
Bibi Mary Nsemwa, ni mkuu
wa Idara ya Ushawishi na Ujenzi wa
Nguvu za Pamoja katika Mtandao
wa Jinsia Tanzania (TGNP), anasema
asilimia kubwa ya wananchi wa
vijijini wanaoathirika na upatikanaji
wa habari ni wanawake.
Bibi Nsemwa alisema wanawake
wanahitaji kuhabarishwa kuhusiana
na kilimo, ujasiriamali, sheria
ya ardhi na mambo mbalimbali
yanayoendelea mijini na duniani,
lakini haki hiyo wanaikosa kutokana
na kutokuwepo kwa miundo mbinu
inayofika maeneo ya vijijini hususan
barabara kwa ajili ya magazeti.
“Hata kwa familia zenye radio
nyingi zinamilikiwa na wanaume,
hivyo wanawake kukosa taarifa
muhimu ndiyo maana wanazidi
kukandamizwa”.
Bw. Marcossy Albanie wa
Kituo cha Msaada wa Sheria na Haki
za Binadamu yeye anasema “kwa
ujumla wakulima ni kundi lililoachwa
nyuma na hata wakizungumza watu
wanawapuuza na ndiyo maana hata
vyombo vingi vya habari vimeegemea
zaidi mjini, ingawa kisingizio kikubwa
kimekuwa ni miundombinu mibovu
vijijini.
“Suala hili linamfanya mkulima
mdogo abaki kwenye kiza na watu
wachache waendelee kunufaika na
rasilimali za nchi.
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
MAKALA
Soko huria lilivyoathiri upatikanaji
wa habari vijijini
Na Rashid Kejo
Tulikotoka
Nchi ya Tanzania tangu ilipopata
uhuru wake mwaka 1961, ilikuwa
ikitumia mfumo wa vyama vingi hadi
mwaka 1965 ilipoamua kuachana
nao. Hata hivyo mwaka 1992,
Tanzania iliridhia mageuzi makubwa
ya kurejea katika mfumo wa vyama
vingi vya siasa.
Sababu iliyotolewa mwaka 1965
wakati wa kuachana na vyama vingi
ni kwamba pamoja na mambo
mengine, vyama vya upinzani
ambavyo vilikuwapo kama vile
African Independence Movement
(AIM) na People’s Democratic
(PDP), havikuwa na nguvu.
Lakini pia wakati ule, kulikuwa na
vuguvugu kubwa la mataifa mengi
ya Afrika kuendeshwa chini ya
utawala wa chama kimoja kutokana
na kile kilichoelezwa kwamba ni
kuleta umoja wa kitaifa na kuondoa
mifarakano na migogoro kwa lengo
la kujiletea maendeleo.
Licha ya kuwa na chama kimoja
kilichokuwa kimeshika hatamu, hata
nyanja nyingine kuu na muhimu za
kiuchumi na kijamii, kwa kiwango
kikubwa zilikuwa chini ya umma.
Vyombo vya habari kadhalika,
vilikuwa katika mfumo dola. Redio,
televisheni (kwa Zanzibar) na
magazeti, ama vilimilikiwa moja
kwa moja na Serikali, taasisi zake au
chama na jumuiya zake.
Tunakumbuka vyombo kama
Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD),
Sauti ya Tanzania Zanzibar (STZ),
Magazeti ya Daily News/Sunday
News, Uhuru/Mzalendo, Mfanyakazi
na Mkulima wa Kisasa.
Kutokana na uchache na umiliki
wake, maudhui ya vyombo hivi
yaliratibiwa na dola yakilenga
masuala kadhaa ambayo Serikali
ilikuwa imeyapa kipaumbele.
Pamoja na changamoto zake,
habari za wakulima zilipata fursa
katika vyombo hivyo. Achilia mbali
gazeti, kulikuwa na vipindi vya redio
vya Mkulima wa Kisasa ambavyo
vilitoa mafunzo na maelekezo
mbalimbali ya kilimo bora.
Kulikuwa pia na mkakati maalumu
kupitia Taasisi ya Vielelezo wa
kupeleka sinema vijijini kuelimisha
wakulima juu ya ukulima na
ufugaji bora. Kimsingi, kulikuwa na
upatikanaji wa taarifa hasa zile za
msingi kwa umma wa vijijini.
Wahenga walisema, kila masika
yana mbu wake. Katika mabadiliko
ya mwaka 1992 yaliyoruhusu mfumo
wa vyama vingi na soko huria,
Serikali ilijitoa katika biashara na
kulegeza masharti hivyo kuiwezesha
sekta binafsi kushiriki moja kwa
moja katika masuala ya kiuchumi
na kijamii. Mabadiliko yalichochea
kuanzishwa kwa Sera ya Habari na
Utangazaji ya mwaka 1993.
Hata hivyo, haikujitoa katika
usimamizi na uendeshaji wa vyombo
vyake vya habari, bali iliruhusu sekta
binafsi nayo kuingia katika biashara
hiyo. Hivyo, kuanzia mwaka 1992,
magazeti, vituo vya televisheni
na redio na baadaye mitandao ya
mawasiliano vilianza kwa kasi.
Tofauti na awali ambako
mwelekeo wa habari ulilenga zaidi
propaganda, safari hii mtazamo
ulikuwa wa kibiashara zaidi na hali
hiyo imekuwa na athari kubwa katika
upatikanaji wa habari za vijijini.
Kutokana na msukumo huo wa
nguvu ya soko, vyombo ambavyo
vilishindwa kujiendesha kibiashara
vilikufa na hivyo ndivyo ilivyotokea
kwa Gazeti la Mkulima wa Kisasa.
Vipindi vingi vilivyoanzishwa katika
redio na televisheni vililenga zaidi
kuwavutia watangazaji (advertisers).
Kwa upande mwingine, asilimia
kubwa ya magazeti na machapisho
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
husomwa zaidi mijini ambako
usambazaji ni rahisi na kiwango cha
kujua kusoma na kuandika ni kikubwa
na hilo likawa na athari kubwa kwa
upatikanaji wa habari za vijijini.
Hiyo
ilimaanisha
kwamba
wakulima na wananchi wengine
waishio vijijini walianza kupewa
habari ambazo hazikuwa na uwiano
wa moja kwa moja na matatizo au
vipaumbele vyao.
Kwa mfano, mwaka 1995
wakati taifa likiwa katika kampeni
za kwanza tangu kurejeshwa kwa
mfumo wa vyama vingi, baadhi ya
vituo vya televisheni vilitumia fursa
hiyo vibaya kwa kuonyesha picha za
mauaji hivyo kuwatishia wananchi.
Mabadiliko makubwa
Hata hivyo, kadri miaka inavyosonga
kumekuwa na mabadiliko makubwa.
Kukua kwa teknolojia ya mawasiliano
na dhana ileile ya soko kumevifanya
vyombo vya habari kuanza kubaini
umuhimu wa kulitazama soko la vijijini
waliko asilimia 80 ya Watanzania.
Halmashauri za wilaya na
wawekezaji wengine wa ndani
wameanzisha redio za jamii
(community radio) ambazo zinatoa
huduma ya habari katika maeneo
yao. Hili limekuwa na mchango
mkubwa kwa wananchi wa vijijini
kwani taarifa, kero na shida zao
zimekuwa zikipata fursa ya kusikika.
Lakini siyo kusikika tu, kumekuwa
na fursa kubwa zaidi ya kupata
habari zinazokidhi mahitaji yao
kwa kiwango kikubwa na hivyo
kuchochea maendeleo yao.
Ingawa wilaya zilizoanzisha radio
hizi za jamii ni chache mno, lakini
wilaya zilizobahatika kuwa na redio
hizi, zimekuwa zikitumia fursa hiyo
kufikisha ujumbe muhimu katika
maeneo husika kama vile bei ya
bidhaa na huduma nyingine muhimu.
Endelea Uk wa 11
7
MFUMO WA TAARIFA ZA MASOKO WA MVIWATA
(MAMIS)
ANA KWA ANA/MAKALA
PATA BEI ZA MAZAO KWENYE SIMU YAKO POPOTE ULIPO!!
Jinsi ya kupata taarifa kwenye simu yako:
Taarifa ya BEI ZA MAZAO
1. Andika neno BEI acha nafasi
2. Andika zao unalotaka bei yake mfano; MAHINDI
3. Kisha tuma kwenda namba 0654 555 884
Taarifa ya WAUZAJI
1. Andika neno NANUNUA acha nafasi
2. Andika zao unalotaka kununua mfano; MAHINDI
3. Kisha tuma kwenda namba 0654 555 884
Taarifa ya WANUNUZI:
1. Andika neno NAUZA acha nafasi
2. Andika zao unalotaka kuuza mfano; MAHINDI
3. Kisha tuma kwenda namba 0654 555 884
Masoko yaliyopo mpaka sasa:
MOROGORO, TAWA, TANDAI, NYANDIRA, KIBAIGWA, DODOMA, IGUNGA, TABORA, SHINYANGA,
MASWA, BARIADI, BUKOMBE, KAHAMA, KILOMBERO (ARUSHA), KARIAKOO, BUGURUNI, TEMEKE,
IGURUSI (MBEYA), MKURANGA, MAKAMBAKO, SIMANJIRO, TAVETA, MKATA, IGAGALA, MATAI
(RUKWA), KASANGA, HIMO, HOLILI, n.k
Mazao yaliyo kwenye mfumo huu:
MAHINDI, MCHELE, MAHARAGE, CHOROKO, KUNDE, MBAAZI, NJEGERE, MTAMA, UWELE, ULEZI,
UFUTA, ALIZETI, NDIZI MBIVU, NDIZI MBICHI, MAGIMBI, MUHOGO, NANASI, CHUNGWA, PAPAI,
EMBE, PARACHICHI, NYANYA, VITUNGUU MAJI, VITUNGUU SAUMU, TANGO, KAROTI, KABICHI,
HOHO, LUBABU, SELELI, BITRUTI, ZUKINI, SALADI, KOLIFLAWA, TANGAWIZI, PILIPILI MTAMA,
MDALASINI, ILIKI.
...meseji moja kwa kila zao moja
Kwa Mawasiliano zaidi piga SIMU NAMBA 0659250317
8
imedhaminiwa na;
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
MAKALA
Taaluma ya habari ni wito
Na Susuma Susuma
V
yombo vya habari ni jina
la jumla la mfumo wa
mawasiliano unaojumuisha
utangazaji wa redio, televisheni,
majarida na magazeti. Vyombo
hivi vina wajibu mkubwa wa
kuhudumia matakwa ya jamii katika
maisha yao ya kila siku. Vyombo
vya habari vinaelimisha, vinatoa
burudani na kutoa changamoto
kwa wananchi na viongozi kuhusu
mambo mbalimbali.
Kadhalika taaluma ya habari ni
tasnia nyeti inayoheshimika katika
jamii yoyote inayothamini ustaarabu,
umoja na utangamano wa kitaifa.
Kuandika
makala
kwenye
magazeti, kusoma taarifa ya habari
au utayarishaji wa vipindi vya siasa,
jamii, utamaduni, dini, burudani ama
matukio yanayohitaji jamii kupewa
taarifa, ni shughuli zinazohitaji
ushirikiano wa kutosha baina ya
wadau yaani waandishi, watoa habari
na walaji (wasikilizaji/wasomaji).
Kwa mantiki hiyo, ushirikiano
madhubuti kati ya wadau wa habari
na waandishi wa habari ni nguzo ya
maendeleo katika jamii.
Aidha,
kufanikisha
masuala
haya kunahitaji umakini, weledi,
mazingatio ya kufuata miiko, maadili
na heshima kwa mwandishi ama
mtangazaji husika.
Utendaji kazi wa vyombo
vya habari
Ukilinganisha miaka 50 iliyopita hali
ya utendaji kazi wa vyombo vya
habari na hali ilivyo hivi sasa nchini
kwetu ni tofauti kabisa.
Uandikaji wa habari, makala,
utangazaji na utayarishaji wa vipindi
hivi sasa hauzingatii ujuzi, taaluma na
kuheshimu miiko, kama ilivyokuwa
miaka ya awali.
Fani hii imeshuhudia watu
wanahitimu uandishi wa habari ngazi
ya shahada ya kwanza au ya uzamili,
lakini bado wakashindwa kuandika
habari kwa usahihi.
Kwa
mfano
eneo
moja
linalowashinda ni jinsi ya kufahamu
mahitaji
halisi
ya
wasomaji,
wasikilizaji ama watazamaji wao,
kushindwa kufahamu habari ilipo
ama kushindwa kutofautisha habari,
uzushi na fitina.
Wapo wanaosema fani hii ni
rahisi kuliko zote na hawa ndiyo
wanaovamia fani hii na kudhani
kwamba wanafanya vizuri bila
kufahamu kuwa wanachangia kuua
taaluma.
Fani hii siyo rahisi kama
inavyodhaniwa na wengi, na pengine
ndiyo maana kila kukicha vyombo
vya habari vinalaumiwa kwa kukiuka
miiko na maadili kwa kuwa wengi
wanaamua kujiunga wakidhani
ni kuandika tu, matokeo yake
wanafanya upotoshaji.
Tumeshuhudia pia utitiri wa
vyombo vya habari vinavyoanzishwa
kila leo, lakini cha kushangaza vingi
vinaanzishwa mijini na kuhudumia
watu wa mijini tu na kuwaacha
kando watu waishio vijijini.
Kwa mujibu wa takwimu za
Msajili wa Magazeti mpaka sasa
amekwishasajili zaidi ya magazeti
na majarida 350 ingawa ni asilimia
15 tu ya machapisho hayo ambayo
yanaonekana mitaani kwa wakati huu
na asilimia kubwa yakiwa mijini. Idadi
kubwa ya magazeti yaliyosajiliwa
yanamilikiwa na watu au makampuni
binafsi isipokuwa magazeti ya ”Daily
News, Sunday News na Habari leo”
ambayo yanamilikiwa na Serikali na
gazeti la Uhuru linalomilikiwa na
chama tawala CCM. Ukipekuwa
kwa undani utendaji kazi wa
magazeti haya sasa yako kibiashara
zaidi kinyume na matarajio ya kutoa
huduma ya kuhabarisha umma.
Vyombo
vya
habari
vinapoanzishwa vikiwa na mlengo
wa kibiashara zaidi, ni moja ya
sababu inayochangia vyombo vingi
virundikane mjini ambako wamiliki
wanaamini watauza na kupata
matangazo ya kutosha. Na hoja hapa
ni Je, jamii ya huko vijijini ambako
biashara ya radio, televisheni na
magazeti hazilipi, itafikiwaje na habari
zenye kuchochea maendeleo?
Kufanya hivi vyombo vya habari
vinakiuka sheria na kuwanyima haki
Endelea Uk wa 10
MVIWATA katika kusaidia wakulima kupaza sauti zao, imekuwa ikiwawezesha wanahabari
kuyafikia maeneo ya vijijini na kuchukua habari za kero zao
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
9
MAKALA
Taaluma ya habari ni wito...
Inatoka uk. wa 9
ya msingi wananchi wa vijijini.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania (1977) ambayo ilifanyiwa
marekebisho mwaka 1984, imeweka
kifungu maalum kinachotaja wazi
kuwa habari ni haki ya msingi ya raia.
Kifungu hicho cha 18 cha Katiba
kinasema:
(1) Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila
mtu yuko huru kuwa na maoni
yoyote na kutoa nje mawazo
yake, na kutafuta, kupokea na
kutoa habari na dhana zozote
kupitia chombo chochote bila
ya kujali mipaka ya nchi, na
pia uhuru wa mawasiliano yake
kutoingiliwa kati.
(2) Kila raia anayo haki ya kupewa
taarifa wakati wowote kuhusu
matukio mbalimbali nchini na
duniani kote, ambayo ni muhimu
kwa maisha na shughuli za
wananchi; na pia juu ya masuala
muhimu kwa jamii.
Wajibu wa vyombo vya
habari
Njia muhimu za kuwezesha
wananchi kufurahia haki ya kupasha
na kupashwa habari na kujieleza
kwa kutoa maoni hadharani bila
bughudha,vitisho na ukandamizwaji
ni kupitia vyombo vya habari.
Kutokana na umuhimu wa kipekee
wa haki hii ya msingi, nafasi ya
vyombo vya habari katika utekelezaji
wake pia ni ya kipekee. Kwa kuwa
vyombo vya habari vinawawezesha
wananchi kutumia haki hii ili isibaki
nadharia au kwenye maandishi tu,
hakuna budi wamiliki wa vyombo vya
habari pamoja na serikali, watambue
na kukiri kwamba nafasi yao ni ya
kutoa huduma au mahitaji ya lazima
kwa jamii, huduma kwa umma.
Hadhi ya huduma ya kijamii
inazidi sana ile ya bidhaa ambazo
huuzwa kuingiza faida. Ndiyo maana
wajibu wa wamiliki wa vyombo vya
habari kwa jamii ni mkubwa kuliko
wa mfanyabiashara ama mwekezaji
ambao msukumo wao mkubwa ni
10
kutengeneza faida.
Hata vyombo vya habari vya
serikali vinapaswa kuwajibika kwa
umma na sio utashi wa kisiasa wa
wanasiasa na watawala.
Wanahabari pamoja na kwamba
huajiriwa na wamiliki wa vyombo,
bado huwajibika kwa umma. Na
ndiyo maana ili vyombo vya habari
viweze
kutekeleza
majukumu
yao, hakuna budi kwa wahariri na
wanahabari kuwa na uhuru wa
kutosha kukusanya, kuchambua
na kusambaza habari bila woga,
shinikizo au ushawishi wa wamiliki
na washiriki wao kibiashara.
Habari ni huduma
Kazi ya uandishi wa habari ni fani
ambayo pamoja na kuwa na ujuzi
lakini inahitaji zaidi wito. Ni fani
ambayo inahitaji zaidi mtu kutanguliza
utu na upendo ama dhana ya kutoa
huduma kuliko malipo ama kufanya
biashara. Ni fani isiyojali sana malipo
yenye kulingana na kadhia, ugumu
wala masuala mengine kwa kuwa
kuna wakati unakuwa unashughulikia
tatizo la kijamii iliyo masikini ambayo
malipo yake ni asante.
Kinachosikitisha zaidi ni kuona
baadhi ya waandishi wa habari
wakishabikia zaidi kuandika habari
za migogoro na kuwachafua watu,
wakati mwingine wakiishia kudai
posho bila hata kuandika chochote.
Hali hii inaonesha walivyokosa
ushirikiano na jamii.
Pia
zipo
sheria
ambazo
zinaonekana kukandamiza uhuru wa
vyombo vya habari nchini, ambazo
wanahabari wamekuwa wakizipigia
kelele
kwa
kuitaka
serikali
kuzirekebisha ama kuzifuta kabisa.
Hizi ni pamoja na sheria ya magazeti
ya Tanzania ya mwaka 1976 ambayo
inampatia uwezo waziri anayehusika
na habari wa kulifungia gazeti lolote
lile kama ataridhika kuwa limekiuka
kwa kiasi kikubwa matakwa ya sheria
hiyo. Sheria hizi pia zinakwamisha
upatikanaji wa habari sahihi zenye
maslahi umma.
Mfano halisi ni wa taarifa
zinazohusiana na kashfa kwenye
migodi ya madini na kwenye sekta ya
uwindaji wanyama kwenye mbuga za
wanyama ambazo zinaakisi uchumi
wa nchi.
Serikali inapaswa kupitisha sheria
rafiki kwa vyombo vya habari na
ambazo zinaweka mazingira huru ya
upatikanaji wa habari, kwani kuvifunga
minyororo vyombo vya habari ni
kuwafunga minyororo wananchi.
Kwa upande mwingine wapo
waandishi wa habari wanaotishiwa
maisha pale wanapofuatilia ili kupata
habari za kina kuhusiana na jambo
fulani lenye maslahi kwa jamii. Lakini
hiyo siyo sababu ya wao kufanya
shughuli zao kinyume cha sheria na
maadili ya taaluma yao kama vile
kutoa na kupokea rushwa, upotoshaji
na udanyanyifu, uchochezi, ushabiki,
kutunga ama kutia chumvi habari.
Hata hivyo changamoto ni sehemu
ya maisha, ni chachu kwa maendeleo
yoyote, wanahabari ni vyema
tukajenga tamaduni ya kwenda
vijijini kuzungumza na kutangaza
habari za mafanikio, ubunifu, uzoefu
na mbinu wanazotumia wanavijiji
kutatua changamoto za maisha yao
ya kila siku.
Kwa
kuwa
tumeamua
kuwatumikia
wananchi
wenye
uhitaji wa huduma yetu, hatuna
budi kuzikabili changamoto zote
za kutafuta, kuandaa na kuzifikisha
habari kwa wadau bila kujali
zinapatikana kutoka mazingira yenye
changamoto nyingi.
Kwa upande mwingine liko kundi
dogo la wanahabari nchini ambao
wamepungukiwa utu na upendo,
wametanguliza zaidi maslahi binafsi,
ndiyo maana wameigeuza fani hii
kuwa biashara badala ya huduma
kwa jamii. Kundi hili japokuwa ni
dogo lakini laweza kuwa na madhara
makubwa kwa jamii hasa kipindi hiki
ambao vitendo vya ufisadi vinazidi
kushika kasi ndani ya nchi yetu.
Wakialikwa kwenda kuchukua habari
Endelea Uk wa 11
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
MAKALA
Soko huria lilivyoathiri...
Inatoka uk. wa 7
Inawezekana bado kuna vikwazo
vya hapa na pale katika kuwafikia
wananchi wa vijijini walio wengi, lakini
muhimu ni kuviimarisha zaidi vyombo
hivi ili walau viweze kuziba pengo
lililosababishwa na kutoweka kwa
majarida kama ya mkulima wa kisasa.
Mamlaka za miji na wilaya nchini
ni mali ya wananchi kupitia mabaraza
ya madiwani ambao wanatokana na
kura za watu katika ngazi za kata.
Kwa maana hiyo basi ni fursa kwa
viongozi hawa wawakilishi wa umma
(madiwani), kuimarisha usimamizi
wa vituo vya redio na televisheni
vinavyomilikiwa na halmashauri zao
ili viweze kukidhi matakwa ya jamii
husika, ziwe za wakulima, wafugaji,
wavuvi, wachuuzi au wengineo.
Hii ni moja ya hatua muhimu
zinazoweza kuwarejesha wazalishaji
wadogo wa sekta mbalimbali nchini
katika dunia ya mawasiliano.
Intaneti na simu za mkononi
Tunapozungumzia habari, hatuwezi
kuacha kuzungumzia njia nyingine
za kisasa za mawasiliano kama vile
intaneti na simu za mkononi. Hizi kwa
ujumla wake zimekuwa na mchango
mkubwa kwa wananchi wa vijijini
katika mambo mbalimbali.
Intaneti kwa mfano, imewawezesha
wananchi kutafuta masoko, masomo
na kuwasiliana kwa sababu mbalimbali
na taasisi, ndugu, jamaa na marafiki zao
walio mbali.
Zamani ilikuwa ni gharama kubwa
na usumbufu kuwasiliana kwa njia ya
barua na ndugu walio mbali. Lakini
sasa, katika baadhi ya maeneo ya
vijijini kuna vituo vya mawasiliano
ambako wananchi huenda na kupata
huduma hizo za mtandao (simu/
intaneti) na hivyo kupata taarifa
mbalimbali za shughuli zao na pia
kuwasiliana na watu mbalimbali.
Magazeti mengi ya ndani na
nje na hata redio zimeunganishwa
pia katika mitandao hii ya intaneti,
hivyo wananchi popote walipo
wanaweza kusoma habari za leoleo
hivyo kujiweka katika nafasi nzuri ya
kuujua ulimwengu na yanayoendelea
na kutumia taarifa hizo kujiongezea
maarifa na kujiendeleza.
Njia hii ya simu ndiyo imekuwa
na athari chanya kubwa. Idadi kubwa
ya Watanzania mijini na vijijini hivi
sasa wanafaidika kwa huduma hii
iwe moja kwa moja au kupitia kwa
ndugu na jamaa zao.
Upashanaji wa habari ulikwaza
mambo mengi ya watu waishio
vijijini lakini baada ya mapinduzi ya
teknolojia hii, si ajabu hivi sasa kwa
mfano, mtu aliye kijijini kumweleza
au kumpa taarifa aliye mjini juu ya
tukio lililotokea huko huko mjini.
Mara ngapi tumesikia watu
waishio Dar es Salaam wakipewa
taarifa za msiba uliotokea hukohuko
Dar es Salaam na mtu aishie
kijijini?
Kimsingi
mawasiliano
hayo yamevunja umbali baina ya
watu wa maeneo haya. Japokuwa
haya yanatokea kwenye maeneo
machache mno ya vijijini ambayo
yamebahatika kuunganishwa na
huduma za simu za mkononi.
Mapinduzi
mengine
chanya
yaliyotokana na uwepo wa mawasiliano
haya ya simu ni utumaji na upokeaji wa
fedha kupitia mitandao ya simu.
Usumbufu wa kuwatumia wazazi
kijijini fedha au kuwalazimu wakulima
na wafanyabiashara kusafiri kwenda
mjini au kijijini kununua au kuuza
bidhaa siku hizi hauna ulazima. Baada
ya kuingia makubaliano, mkulima
anaweza kufungasha mazao yake na
kuyatuma mjini na kutumiwa fedha
kwa njia ya simu na hayo hufanyika
ndani ya muda mfupi mno. Zaidi ya
hayo huduma za mawasiliano ya simu
zimepanua wigo wa ajira kwa vijana
vijijini na kuongeza kipato, hivyo
basi wananchi wanapaswa kuitumia
vyema fursa hiyo kwa kuifanya kuwa
kichochocheo cha maendeleo yao.
Taaluma ya habari
ni wito...
Inatoka uk. wa 10
kijijini, swali la kwanza wanalouliza ni
watalipwa? nani atawalipa? kiasi gani
watalipwa? Wakishapewa majibu
kuwa hakuna malipo kwa kuwa
kazi hiyo ni sehemu ya utekelezaji
wa majukumu yao, wanaishia kutoa
visingizio vya kutoenda kufanya kazi
hiyo.
Wanahabari
tunapaswa
kujitambua kuwa sisi ni nguzo
muhimu ya maendeleo katika
jamii hivyo tunatakiwa kujenga
ushirikiano madhubuti baina yetu
na wadau wa habari wakati wa
kutekeleza majukumu ya kuipasha
habari jamii kwa uaminifu na
kudhihirisha kuwa tulioko kwenye
taaluma hii tuna wito.
Aidha ni muhimu kwa umma
kuwa na imani na wanahabari
kuwa wanachofanya ni sehemu
ya utekelezaji wa majukumu
kama ilivyo kwa watumishi
wa sekta nyingine na kwamba
hawana sababu ya kuwaogopa,
kujenga chuki ama kuwapa taarifa
za uongo na uchochezi, bali
washirikiane nao kwa ukaribu.
Ni vyema kila kundi likajali na
kuheshimu uhuru wa kutoa na
kupata habari kama ilivyo ndani
ya katiba ya nchi.
Jihadhari na
maambukizo ya
UKIMWI
jikinga na umlinde
mwenzako
Mwandishi wa Makala hii ni
Mhariri wa Habari wa Gazeti
la Mwananchi
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
11
KAMERA
KAMERA YA MVIWATA MITANDAONI
Wakulima wa kata ya Mlangali wilayani Ludewa wakioneshana
jambo lililowavutia kwenye gazeti la Pambazuko linaloandika habari
za wakulima na kusambazwa vijijini
Bibi HotensiaThomas, mwenyekiti wa Bodi ya Soko la Wakulima
Nyandira akisikiliza swali kwa mmoja wa wadau wa masoko ya
Igurusi, Matai na Kasanga walipofanya ziara sokoni hapo Julai 21,
2011
Moja ya mikutano ya mitandao ya wakulima ambayo imekuwa
ikitumika kupashana habari vijijini
Wana-MVIWATA walioshiriki Tamasha la Jinsia Septemba 2011
wakimsikiliza mwenzao wakati wa majadiliano
Picha ya pamoja ya baadhi ya viongozi na watumishi wa MVIWATA
na wawakilishi wa ubalozi wa Ireland nchini Bibi Aileen D’donovan,
Dkt Sizya Lugeye na Bw.Vicent Akuluyuka (wa nne hadi wa sita
kutoka kushoto waliosimama), baada ya ujumbe huo kutembelea
makao makuu ya MVIWATA yaliyoko Morogoro Julai 5, 2011.
Wana-MVIWATA Kiteto Manyara walioshiriki mafunzo ya kujengea
uwezo viongozi Julai 28-29, 2011, wakiwa na baadhi ya watumishi
wa MVIWATA taifa waliowezesha mafunzo hayo
12
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
KAMERA
KAMERA YA MVIWATA MITANDAONI
Ukosefu wa habari sahihi za masoko vijijini unasababisha bidhaa za
wajasiliamali kama hawa wa Kwekanga Lushoto kukosa soko
‘Natangaza kazi za mikono’, ndivyo anavyoelekea kusema mama
huyu mkazi wa kijiji cha Kwalei wilayani Lushoto
Wakulima wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kushiriki
Jukwaa la Wakulima mkoani Ruvuma
Bibi Elizabeth Lagwen (kulia) Mwenyekiti wa mtandao wa msingi
Mamire Babati Vijijini akiwasikiliza wageni kutoka shirika la TRIAS
Ubeligiji waliomtembelea kujifunza shughuli anazozifanya
Wanawake jamii ya wafugaji wilayani Monduli, wakishiriki kazi ya
kuchimba msingi na kuweka mawe ya msingi ya jengo la kukusanyia
la kituo cha kibiashara
Licha ya kuwa na historia ya ufugaji pekee, jamii ya Wamasai sasa
wamebadlika na kuanza kushiriki kilimo kama wanawake hawa
walivyokutwa na kamera yetu wakipanda mazao shambani
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
13
KUTOKA MITANDAONI
Maonesho ya NaneNane 2011
Wakulima wazungumzia matumizi na faida
za bidhaa walizoonesha
Na Goodness Mrema, Morogoro
M
tandao
wa
vikundi
vya wakulima Tanzania
(MVIWATA)
katika
kuhakikisha kwamba unatekeleza
vyema majukumu yake umekuwa
na utaratibu wa kuwawezesha
wakulima toka mikoa mbalimbali
kushiriki kuonesha bidhaa zao
kwenye maonesho ya kilimo
maarufu kama NaneNane.
Mwaka 2011 katika maonesho
hayo ya wakulima MVIWATA
iliwawezesha wakulima zaidi ya 40
kushiriki maonesho hayo kwenye
viwanja vya Mwalimu Nyerere
Morogoro na Themi Arusha, kwa
lengo la kuwapatia fursa ya kujifunza,
kubadilishana uzoefu na kutangaza
bidhaa zao. Katika maonesho hayo
MVIWATA ilipata ushindi wa kwanza
kwa upande wa vyama na mashirika
yasiyo ya kiserikali kwenye uwanja
wa maonesho ya NaneNane kanda
ya Mashariki wa Mwalimu Nyerere
Morogoro na katika kanda ya
Kaskazini kwenye viwanja vya Themi
Arusha na kukabidhiwa zawadi ya
Kombe na Cheti vilivyotolewa na
Waziri Mkuu Bw. Mizengo Pinda.
Aidha kwenye viwanja vya Themi
Arusha mkulima Bw. Richard Kipara
ambaye ni katibu wa Mtandao wa
Vikundi vya Wakulima Ekenywa
(MVIWAEKE)
alishinda
kuwa
‘Mkulima Bora’ wa wilaya mpya ya
Arusha Vijijini.
Katika maonesho hayo mfugaji
Bw. Moses Ndoipo kutoka wilaya ya
Longido, alileta mbuzi bora aina ya
Isiolo wa uzito wa kilo 240 aliyekuwa
anauzwa Sh. 300,000 na kuwa
kivutio kwa wageni waliotembelea
maonesho.
Miongoni mwa wakulima waliopata
fursa ya kushiriki maonesho haya
ya NaneNane
kwenye viwanja
vya Mwalimu Nyerere Morogoro,
walielezea umuhimu wa bidhaa
walizoonesha na faida ya maonesho
kwa ujumla.
Kakao na Mawese
Bibi Lain Mwakatundu kutoka
Kyela, Mbeya alikuwa na zao la
mawese na kakao ambapo
alisema usindikaji wa mawese
unawezesha utengenezaji wa bidhaa
mbalimbali muhimu kama vile sabuni
ya kufulia na kuogea.
Lain Mwakatundu
“Vile vile kutokana na mawese
unaweza kupata mbosa ambayo
hutengeneza mafuta ya kupikia
na kupaka. Mafuta haya ya kupaka
yanafaida kubwa ikiwemo ya
kuponya mba wa ngozi katika mwili
wa binadamu. Aidha magamba ya
mawese hutumika kwa ajili ya kuni.
Kwa upande wa zao la kakao
alisema lina matumizi mengi
ingawaje matumizi yanayofahamika
zaidi kwa watu ni utengenezaji
Endelea Uk wa 15
Mwenyekiti wa MVIWATA Morogoro Bw. Stanford Chabonga aliyenyanyua juu kikombe, akiungwa mkono na wana-MVIWATA wenzake
kusherehekea ushindi
14
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
KUTOKA MITANDAONI
Inatoka uk. wa 14
wa kinywaji na kitafunwa aina ya
chocolate. Akaongeza kuwa “ndani
ya tunda la kakao kuna mbegu zenye
ladha ya sukari ambazo hutumika
kutengeneza juisi lakini pia juisi hiyo
waweza kuichachusha na kupata
kilevi baada ya kuiweka kwa muda
wa siku tatu hadi nne.”
“Mbegu hizi za kakao pia
zikikaushwa na kusagwa hupatikana
unga laini ambao unafaa kwa
matumizi mengi ikiwemo kuweka
kama kiungo kwenye mboga na
wengine hutafuna unga pekee maan
unaradha nzuri,” anafafanua.
Bibi. Mwakatundu anafafanua zaidi
kuwa zao la kakao ni dawa nzuri
ya kupunguza kasi ya ugonjwa wa
kisukari mwilini na pia hupunguza
mafuta ndani ya mwili wa binadamu,
hivyo anawahimiza watanzania
kulitumia zaidi.
Anaeleza kuwa katika mkoa wa
Mbeya hususan wilaya ya Kyela mazao
ya Kakao na Mawese hulimwa kwa
ajili ya chakula na biashara japokuwa
soko lake kwa sasa siyo zuri. Hata
hivyo anaongeza kuwa maonesho ya
mwaka huu yamemsaidia kupanua
wigo wa soko kwani hivi sasa
amepokea maombi ya wateja wengi
wanaohitaji bidhaa na wengine
wameomba aende kuwafundisha
kilimo cha mazao hayo.
Tiba asili
Mzee Hassan Nundu kutoka
kijiji cha Chamkoroma wilaya ya
Kongwa - Dodoma, yeye alionesha
dawa za asili zinazotokana na
magome na mizizi ya miti ambazo
zinaaminika
kutibu
magonjwa
mbalimbali ya binadamu kama vile
meno, tumbo, athma pamoja na
kideri cha kuku.
Akielezea matibabu ya ugonjwa
wa vidonda vya tumbo, anasema
mgonjwa anayetumia dawa hiyo
anapona kwa muda mfupi hata kama
vidonda ni vya muda mrefu. “Dawa
hii ambayo ni mchanganyiko wa
mizizi ya miti mbalimbali, mtumiaji
huchanganya na maziwa mabichi
kwa kuweka kijiko kimoja cha
dawa katika kikombe cha maziwa
na kunywa mara tatu kwa siku kwa
muda wa siku kumi na tano tu.”
“Dawa nyingine ni ya fangasi
ambapo fangasi hawa huwa tumboni
na kwenye mapacha ya vidole vya
miguu kutokana na joto linalokuwepo
ndani ya kiatu kufuatia msuguano
wa miguu ya mtu anapotembea.
Dawa hii ya unga inampasa mgonjwa
kuiweka kwenye maji baridi na kisha
kuichuja ili kupata mabaki ambayo
atayapaka sehemu zilizoathirika na
baadaye kunywa dawa iliyochujwa
mara tatu kwa siku kwa muda wa
siku tatu na atapona kabisa.”
Bw. Nundu anafafanua kuwa
athma ni ugonjwa ambao hauna tiba
hospitalini bali hutulizwa lakini yeye
anayo dawa ya kutibu ugonjwa huu
ambayo inapatikana kwenye vipaketi
vitatu. Mgonjwa anapaswa kuiloweka
na kuichuja kisha kunywa mara mbili
kwa siku asubuhi na jioni.
“Ninawashauri
Watanzania
kurudia dawa zao za asili
zinazotokana na mizizi na magome
ya miti kwani hazina kemikali
zitakazowadhuru kiafya tofauti na
dawa za hospitalini ambazo nyingi
sasa ni bandia na kuongeza kuwa
anazo dawa nyingi za asili zinazotibu
maradhi ambayo hayawezi kutibiwa
hospitalini kama vile kukojoa
kitandani pamoja na meno ambayo
mara nyingi hung’olewa badala ya
kutibiwa.
Mzee Nundu anasema maonesho
ya NaneNane ambayo amekuwa
akishiriki yanamsaidia kupata wateja
wapya na kukutana na wagonjwa
aliowatibu miaka ya nyuma ambao
wanashuhudia kuponywa na dawa
zake.
Bibi Hortenzia Thomas kutoka
kijiji cha Nyandira Mvomero, mkoani
Morogoro alifika katika maonesho
hayo kutangaza tiba asili itokanayo
na matunda na mbogamboga
zikiwemo njegere, sereri, cornflower,
maharagwe, redishi, boga, nzukini,
pasili na kabichi.
Anaeleza kuwa kabichi huponya
ugonjwa wa kisukari. Hii ni baada ya
mgonjwa kuchukua mti wa katikati ya
kabichi kuukatakata na kuuchemsha,
kisha kunywa maji yake mara tatu
kwa siku. Pia mboga mboga kama
Radishi na tenepsi hutumika kutibu
vidonda vya tumbo na shinikizo la
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
damu.
Bibi Mwajuma Mwiyoha,
ni mkulima kutoka Chamkoroma
ambaye alifika kwenye maonesho
haya akiwa na zao la Alizeti ambalo
ni maarufu kwa kutengeneza mafuta
ya kupikia. Hata hivyo, kwa mkulima
huyo zao la Alizeti siyo kwa ajili
ya kukamua mafuta pekee bali pia
hulitumia kutengeneza dawa ya
kuhifadhia mazao galán, dawa ambayo
haina madhara kwa watumiaji.
Mwajuma Mwiyoha
“Dawa hii ya kuhifadhia mazao
hutokana na masuke ya alzeti
hutengenezwa
kwa
teknolojia
rahisi tu ambayo mkulima yeyote
anaweza kumudu kwani cha kufanya
ni kuyachoma masuke ya alizeti
kwenye chombo kisafi, yakishaungua
vizuri hutwangwa na kuchekechwa
ili kupata majivu laini ambayo
ndio dawa yenyewe. Dawa hii
hunyunyizwa juu ya magunia yenye
mazao na ina uwezo wa kuzuia
mazao yasishambiliwe na wadudu
kwa muda wa miaka miwili hadi
mitatu.
Bibi. Mwiyoha anasema dawa hii
ni nafuu kwani haimwingizii mkulima
gharama na ni salama kwa afya ya
binadamu.
Ufugaji wa nyuki wadogo
Bw. Hassan Haji kutoka Zanzíbar
ni mkulima mdogo anayefuga nyuki
wadogo wasiouma.
Mkulima huyu ameanza ufugaji wa
nyuki wasiouma miaka 15 iliyopita.
Alianza ufugaji wa nyuki hao kama
mradi wa kiuchumi lakini pia kwa
lengo la kuwahifadhi baada ya kuona
kwamba wako hatarini kutoweka
kutokana ukataji wa miti katika
maeneo ya misitu vitendo ambavyo
vinawafanya viumbe hao kukimbia
na hivyo kizazi hicho kupotea.
Endelea Uk wa 17
15
KUTOKA MITANDAONI
Ludewa wahimizwa kuwekeza
kwenye kilimo cha miti
Na Susuma Susuma, Ludewa
W
akulima
wilayani
Ludewa na nchini kote
wametakiwa kuwekeza
zaidi katika upandaji wa miti
kibiashara ili kuhifadhi mazingira
na kujiongezea kipato kutokana
na soko la miti kuongezeka kila
mwaka.
Wito huo umetolewa na Naibu
Mkurugenzi wa Shirika la Swedish
Cooperative Center (SCC) Kanda
ya Mashariki mwa Afrika Bw. George
Onyango alipokuwa akizungumza na
wakulima wa kata za Mlangali na
Milo wilayani Ludewa katika mkoa
mpya wa Njombe.
Bw. Onyango alikuwa kwenye
ziara ya kukagua maendeleo ya
mradi wenye lengo la kuwawezesha
wakulima wadogo kuwa na uzalishaji
wenye kukuza na kuongeza kipato
na uhifadhi wa mazingira na bioanuai
Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Swedish Cooperative Center (SCC) Kanda ya Mashariki mwa
Afrika Bw. George Onyango (aliyenyosha mkono) akizungumza na wakulima wa kata ya Mlangali
ya chakula wanayolima.
Aidha aliwataka wakulima hao
kuunda mitandao imara itakayofanya
kazi ya kutafuta na kusimamia soko
la mazao ya miti ili kuondokana na
walanguzi ambao sasa wananeemeka
kwenye biashara ya mazao ya chakula
Uharibifu
ya wakulima.
huu tuliufanya sisi katika
Naibu
mkurugenzi
huyo
alisema
licha ya
harakati za kujitafutia riziki, na
kuwaingizia utajiri,
tunaoathirika na uharibifu huu ni sisi, hivyo
kilimo cha miti
ni sisi wenyewe ndiyo tunapaswa kurejesha
kitasaidia
kwa
kiwango
kikubwa
uhai wa mazingira yetu kwa kuwekeza kwenye
katika
utunzaji
upandaji miti na kwa kufanya hivi tutasaidia wa mazingira ya
kupunguza athari za mabadiliko ya
wilaya hiyo ambayo
yameharibiwa
kutokana
tabia ya nchi
na shughuli za kibinadamu
zikiwemo ukataji miti kwa ajili ya
katika
Ziwa Nyasa unaotekelezwa na kupata nishati ya mkaa na kuni.
“Uharibifu huu tuliufanya sisi
Mtandao wa Vikundi vya Wakulima
Wadogo Tanzania (MVIWATA) kwa katika harakati za kujitafutia riziki,
na tunaoathirika na uharibifu
kushirikiana na SCC.
Bw. Onyango alisema biashara ya huu ni sisi, hivyo ni sisi wenyewe
miti na mazao yake, inakuwa kila siku ndiyo tunapaswa kurejesha uhai
na kupanda bei, hivyo kwa kuwekeza wa mazingira yetu kwa kuwekeza
zaidi kwenye upandaji miti wakulima kwenye upandaji miti na kwa kufanya
hao watapata mapato mazuri kuliko hivi tutasaidia kupunguza athari za
hata wanayoyapata kwenye mazao mabadiliko ya tabia ya nchi,” alisema
Bw. Onyango.
Aliwahimiza
wakulima
hao
kutumia vyema elimu ya uhifadhi wa
mazingira, ujasiriamali na usimamizi
wa vikundi inayotolewa kupitia
mradi huo.
Kwa
upande
wake
afisa
anayesimamia mradi huo wilayani
Ludewa Bw.Remmy Urio alisema
matokeo ya mafunzo yaliyotolewa
kwa wakulima yameanza kuonekana
baada ya wengi wao kuanza kupanda
miti kwenye maeneo ya wazi na
wameimarisha usimamizi wa sheria
zinazolinda mazingira.
Bw. Urio alisema wakulima wengi
pia wameibua miradi ya kiuchumi
ikiwemo uanzishaji wa SACCOS
ili kuwawezesha kuboresha kipato
badala ya kutegemea kipato kutoka
kwenye kazi zinazochangia uharibifu
wa mazingira.
Afisa Programu wa MVIWATA
Bw. Laurent Kaburire alisema, utafiti
uliofanywa na MVIWATA kwenye
wilaya zinazounganishwa na Ziwa
Nyasa kwa upande wa Tanzania,
umebaini kwa shughuli nyingi
zinazoathiri ziwa zinatekelezwa
na wavuvi, wafugaji na wakulima
Endelea Uk wa 17
16
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
KUTOKA MITANDAONI
Maonesho ya NaneNane 201...
Inatoka uk. wa 15
Miongoni mwa faida anazozipata
Bw. Haji ni pamoja na kujipatia kipato
kwa ajili ya familia yake kwani kwa
sasa anao wateja wengi wanaotumia
asali ya nyuki hawa wasiouma na
kwamba asali yake ina soko zuri. Kwa
sasa ana jumla ya mizinga 20 ya nyuki
ingawaje changamoto anayokutana
nayo katika kupanua ufugaji huo ni
ugumu kuwapata kutoka msituni
kwani huwa wanajificha sana.
“Ninawashauri
watanzania
kupenda kutumia zaidi asali kwani ni
kinga ya maradhi mengi kwenye mwili
wa binadamu. Hiki ni chakula kizuri
mno hasa kwa watoto, nawaambia
wazazi wasiwape watoto pia badala
yake wawape asali,” anasisitiza.
Ukaushaji
matunda
na
mbogamboga
Bw. Zuberi Sultani kutoka
Korogwe Tanga kwenye maonesho
haya yeye alionesha utaalamu
wa kuhifadhi matunda na
mboga mboga kwa njia
ya ukaushaji. Miongoni mwa
matunda yanayosindikwa ndizi,
mananasi, maembe pamoja na
zikiwemo mbogamboga kama vile
mchunga na kisamvu.
Anafafanua kuwa usindikaji wa
matunda na mboga unafanyika ili
kuyahifadhi na kutumika kwa msimu
wote wa mwaka, wakulima wengi
wa matunda hawanufaiki na kilimo
hicho kwa sababu msimu wa mavuno
matunda hushuka bei na mengine
kuoza kwa kuwa wakulima hawana
ujuzi wa kuyahifadhi.
Anasema ukaushaji huu hutumia
teknolojia rahisi, ambayo yeye
amekuwa akiwafundisha wakulima
wenzake bure ili nao wanufaike.
“Tunakausha kwa kutumia chombo
maalum ambacho hufunikwa na
turubali jeusi juu kwa lengo la
kupunguza ukali wa mionzi ya jua
na kuhakikisha kwamba haileti
madhara kwa watumiaji. Matunda
haya yanapokaushwa huzidishiwa
ubora kwani sukari yake huongezeka
mara dufu ukilinganisha na tunda
linavyokuwa katika hali ya kawaida.”
“Mtanzania yeyote anaweza
kusindika matunda na hata mboga
Watazamaji wakitoka kwenye banda la MVIWATA
kwani si kazi ngumu bali inahitaji
usafi na uangalifu wa karibu ili
kuhakikisha bidhaa inakuwa katika
kiwango cha juu cha ubora ili isilete
madhara kwa binadamu,” anaeleza.
Bw. Sultani anasema kwamba
utaratibu wa kusindika matunda
huanzia katika utafutaji wa matunda
mazuri yaliyoiva kiasi, unayaosha
kuyakata vipande vidogo vinavyoweza
kukauka upesi, kisha kuyaweka
kwenye chombo kinachotumia
mwanga wa jua kukaushia na
baada ya hapo huhifadhiwa kwenye
vifungashio maalum tayari
kwa
kuuzwa.
Utaratibu huu unafanana vile vile
katika mboga za majani ambapo
huoshwa na kuchemshwa kidogo
jikoni kisha huanikwa katika
chombo kinachotumia mwanga wa
jua kukaushia mazao na baada ya
kukauka huwa tayari kufangashwa
kwa ajili ya kuuzwa ama kuliwa.
Usindikaji zao la Muhogo
Bw. Juma Nyamgunda kutoka
Mkuranga Pwani anasema katika
kuhakikisha kwamba zao hili la
muhogo linaongezewa thamani
wakulima wa Mkuranga wameanza
kusindika muhogo na kupata unga
ambao huutumia katika kutengeneza
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
vitu mbalimbali ikiwemo keki, biscuti,
tambi, chinchin, chapati na maandazi
kazi ambayo hufanywa kwa wingi na
kina mama kwa lengo la kuongeza
kipato cha familia.
Bw.
Nyamgunda
anasema
usindikaji unawapa faida kubwa
wakulima
ukilinganisha
na
walivyokuwa wakiuza muhogo ghafi
kwa walanguzi na katika maonesho
ya NaneNane amepata wateja wengi
wanaohitaji kiwango kikubwa cha
unga wa muhogo.
Ludewa
wahimizwa...
Inatoka uk. wa 16
wadogo ambao kipato chao ni
kidogo ama cha wastani.
Alisema katika hatua ya awali ya
miaka mitatu ya majaribio, mradi
unatekelezwa kwenye wilaya mbili
ambazo ni Kyela mkoani Mbeya na
Ludewa mkoani Njombe. Katika
hatua ya pili ya mradi utajumuisha
wilaya za Mbinga mkoani Ruvuma
na Makete mkoani Njombe.
Kwa ujumla mradi unalenga
kuwafikia
na
kuwanufaisha
wakulima,wafugaji na wavuvi
wapatao 15,000 wa hapa nchini.
17
MAKALA
Mtweve: Ubunifu wangu wa redio
umenufaisha wengi
Anamiliki Mlangali Coconut FM
H
atimaye ndoto ya siku
nyingi ya Bw. Ditrick
Mtweve (18) mkazi wa
Kata ya Mlangali wilayani Ludewa
mkoa mpya wa Njombe imeweza
kutimia baada ya kutumia ubunifu
wake kutengeneza mtambo wa
redio unaowanufaisha wakazi
wengi wa wilaya hiyo.
Mtambo huo uliotokana na
kuunganishwa kwa vifaa mbalimbali
kutoka katika redio mbovu na vifaa
vinginevyo kama miti ya mianzi,
boksi na vyuma vya baiskeli, ulianza
kurusha matangazo yake mwaka jana
katika kijiji cha Lufumbu na kwa sasa
matangazo hayo yanawafikia wakazi
wa vijiji sita katika Kata ya Mlangali.
Kwa sasa redio hii ambayo ameipa
jina la ‘Mlangali Coconut FM’ imekuwa
ikitumiwa na viongozi wa vijiji vya
kata ya Mlangali kutangaza taarifa
muhimu kama vile mikutano ya
vijiji, kampeni ya chanjo pia shughuli
muhimu za kijamii.
Vile vile imekuwa kichocheo
kikubwa cha biashara na burudani
kwani watu binafsi hutumia redio
hiyo kutangaza biashara na huduma
wanazotoa bila kusahau wapenzi wa
muziki wa kisasa na nyimbo za injili
ambao pia hupata fursa ya kupiga simu
na kuchagua wimbo waupendao.
Bw. Mtweve ambaye ni mtoto
pekee kwenye familia na yatima
(aliyefiwa na baba) alisema kuwa
alitamani siku moja katika maisha
yake awe mtangazaji maarufu
wa redio kubwa hapa nchini na
ikiwezekana aweze kumiliki redio
yake mwenyewe na mapema mwaka
2009 akiwa kidato cha tatu katika
Shule ya Sekondari ya Lufumbu
ndoto yake ilianza kutimia ambapo
kwa kutumia maarifa madogo
aliyoyapata shuleni alianza kubuni na
kutengeneza mtambo huo wa redio.
“Wakati naanza ilikuwa kama
mchezo, kwanza nilichukua muda
nikitafakari kwanini ‘Microphone’
zisizo na waya zinasafirisha sauti
na kuupeleka katika mitambo.
Baadaye nilichukua kifaa ‘transistor’
kilichotumika katika ‘Microphone’
hizo na vifaa vingine nilivichukua
katika redio mbovu na kuviunganisha,”
alisema Bw. Mtweve. Baada ya kukusanya vifaa
mbalimbali kutoka kwenye redio
mbovu na maeneo mengine pia
alitumia betri za kawaida hatimaye
kufanikiwa kuwasha mtambo wake
na redio yake kuanza kusikilizwa na
wananchi waishio jirani.
Uwezo huu wa redio kusikilizwa
na watu wa jirani ulianza baada ya
Mwanachama na mhamasishaji wa MVIWATA Mlangali akizungumza kwenye kipindi cha
karibu mgeni
18
kuboresha baadhi ya vifaa vyenye
uwezo mkubwa zaidi ili kuwezesha
mawimbi ya sauti kufika mbali zaidi na
hatimaye alifanikiwa kufunga mnara
wa mlingoti wa miti iliyounganishwa
wenye antena ya waya wa kawaida
juu yake na kuutundika juu ya
kilele cha mlima uliokuwa jirani na
nyumbani kwao.
“Haikuwa kazi ndogo kwani
mwanzoni niliweka mtambo huu
nyumbani kwetu ambako ni bondeni
ikawa inasikika nyumba kadhaa za
jirani tu. Ilibidi kutumia muda mwingi
na kuumiza akili ili kuweza kufikia
mafanikio, baadaye nikapata wazo
la kuhamia hapa mlimani kwenye
nyumba ya rafiki yangu ambaye
amenipangishia chumba kimoja,”
alisema Bw. Mtweve alipozungumza
na Pambazuko ndani ya studio yake
kijijini Lufumbu.
Bw. Mtweve alisema anafurahia
ubunifu wake lakini bado anakabiliwa
na changamoto nyingi sana ikiwemo
kutokujua sheria “mpaka sasa redio
hii naimiliki kienyeji kwa lengo la
kukuza kipaji changu na kuiwezesha
jamii inayonizunguka kunufaika na
kipaji hicho, sijui taratibu za kuisajili
zikoje,” alisema Bw. Mtweve.
Tatizo jingine ni kukosa mtaji wa
kuweza kununua vifaa vya kisasa na
kuwa na jengo maalumu la studio ya
utangazaji.
Kwa hivi sasa Bw. Mtweve anaishi
na mama yake baada ya baba yake
kufariki wakati yeyé akiwa na umri
wa miaka 10 na alikuwa akisoma
darasa la tatu wakati huo.
Endelea Uk wa 19
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
MAKALA
Inatoka uk. wa 18
Alisema hali hiyo ya kubakia na
mzazi mmoja imechangia kwa kiasi
kikubwa umasikini katika familia
yao baada ya mama yake kutokuwa
na uwezo wa kifedha na hata afya
yake kutokuwa thabiti kutokana
na maradhi yanayomsumbua na
hivyo wakati mwingine hulazimika
kusimamisha kazi za redio ili
kumsaidia mama yake shughuli za
shamba.
“Redio hii huwa hewani kwa
masaa 24 kila siku kwa kurusha
muziki hewani na salamu, short
time za muziki wa bongo flava na
chaguo la msikilizaji, na inapofika
4.00 usiku hurudi nyumbani na
kuuacha mtambo ukipiga muziki
mpaka alfajiri ninapoingia kuendelea
na vipindi,” alisema Bw. Mtweve.
Awali kabla ya kufikia kiwango
cha kurusha matangazo saa 24,
alikuwa akitumia redio inayotumia
kanda za kawaida na baadaye alipata
redio yenye kutumia ‘memory card’
ambayo imekuwa ikimwezesha
kupiga muziki muda wote. Hata hivyo eneo hili la Mlangali
bado halijafikwia na huduma ya
umeme waTanesco hali inayomlazimu
kutumia betri za kawaida za
redio kuendeshea mtambo wake.
“Nimekuwa nikiwategemea watu
mmoja mmoja ambao wanavutiwa
na huduma hii, kuninunulia betri,
kuna wakati zinapoisha na hakuna
mtu wa kununua ninalazimika kuzima
matangazo kwa siku kadhaa, hadi
ninapoenda kufanya kibarua mahali
Hii ndiyo mitambo ya kurusha matangazo
ya COCONUT FM
na kupata fedha, nitafurahi kama
kijijini kwetu tutapata umeme.”
Wakazi wa vijiji vya kata hiyo
ambao
hawakuwa
wakimiliki
redio majumbani mwao kwa sasa
wameanza kumiliki redio na kusikia
matangazo na burudani kutoka
katika mtambo wa redio ya kijana
huyo. Wafanyabiashara wa Mlangali nao
kwa uchache wameanza kuitumia
fursa ya redio hii kujitangaza na
humlipa kati ya Sh 500 na 1,000 ili
kuweza kurushiwa matangazo yao
redioni kwa siku kiwango ambacho
kijana huyo anasema kuwa kimekuwa
kikimsaidia kwa mahitaji binafsi yeye
na mama yake.
Anasema hata hivyo kuwa kwa
sasa yeye ndiye mtangazaji na fundi
mitambo wa redio hiyo.Anawaomba
wananchi wenye uwezo na ambao
wanaguswa na kipaji chake kumsaidia
kuweza kwenda kusoma katika chuo
cha ufundi stadi (Veta) ili kuongeza
maarifa. Sambamba na hilo, kijana huyu
anaeleza kuwa kamwe ndoto zake
Afisa programu wa MVIWATA Bw. Laurent Kaburire akimtambulisha Bw.Ditrick Mtweve kwa
wajumbe wa Mkutano Mkuu wa 16 wa MVIWATA Oktoba 24, 2011 mjini Morogoro
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
hazitaishia hapo, bali ataendelea
kubuni mbinu mbalimbali na
kuboresha kazi yake hiyo na kiu
yake ni kuona siku moja redio hiyo
inasikika katika wilaya nzima ya
Ludewa.
Bw. Mtweve anaishukuru jamii
inayomzunguka kwani pamoja na
kukosa fedha sambamba na ufinyu wa
elimu ya ufundi alionayo, bado jamii
hiyo imekuwa msaada mkubwa sana
kwake kwani wameweza kutambua
umuhimu wake katika jamii kwa
kumpati redio mbovu ili aweze kutoa
vifaa muhimu kwa kazi yake.
Hii ndiyo studio ya COCONUT FM
Kwa kutambua mchango mkubwa
anaoutoa katika kuhakikisha jamii ya
vijijini inafikiwa na habari, Mtandao
wa Vikundi vya Wakulima Tanzania
(MVIWATA), ulimwalika Bw. Mtweve
na kuwezesha kushiriki kwenye
Warsha ya Kitaifa na Mkutano Mkuu
wa 16 wa MVIWATA uliofanyika
Oktoba 24 na 25, 2011 mjini
Morogoro.
Mojawapo ya mada iliyojadiliwa
kwenye warsha hiyo na kugusa hisia
ni “haki ya upatikanaji wa
habari vijijini” ambapo wakulima
kutoka vijiji mbalimbali walieleza
jinsi ambavyo wanakabiliwa na
changamoto katika kupokea na
kutoa habari katika kutokana na
vyombo vingi vya habari kuegemea
zaidi mijini.
Hivyo washiriki hao walipongeza
ubunifu wa kijana huyo na kuomba
MVIWATA kama taasisi kuendelea
kumuunga mkono na kumtumia
kutangaza zaidi habari za wakulima.
Jambo hilo limetekeleza na hivi sasa
baadhi ya vipindi vya SAUTI YA
MVIWATA vinarushwa kupitia redio
hiyo Mlangali Coconut FM.
19
KUTOKA MITANDAONI
Viongozi wa masoko ya wakulima
wapewa ushauri
Na Susuma Susuma, Morogoro
V
iongozi wa masoko ya
wakulima
wametakiwa
kutojenga uhasama na
viongozi wa awamu zilizopita bali
wawatumie kujifunza na kupata
mbinu za kuyafanya masoko hayo
kuwa endelevu.
Wito huo umetolewa Julai
30,2011 mjini Morogoro na
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi
wa Soko la Wakulima la Kibaigwa
Kongwa mkoani Dodoma Bw.
Richard Kapinye kwenye kikao cha
pamoja cha wakurugenzi wa bodi
za masoko sita yaliyojengwa na
MVIWATA kwenye vijiji mbalimbali
hapa nchini.
Bw. Kapinye alisema “tuepuke
uhasama unaofanywa na wanasiasa
kwamba akishamuondoa mwenzake
madarakani wanakuwa maadui
wanaotafuta kuharibiana kila wakati,
sisi tuwe tofauti tuwatumieni
wenzetu waliotutangulia ili tuweze
kufanikiwa.”
Kadhalika Bw. Kapinye ambaye
pia ni mkulima mdogo na Diwani
wa Kata ya Kibaigwa, aliwataka
wajumbe
wenzake
kutumie
vyema dhamana waliyopewa kwa
kusimamia haki na maslahi ya
wakulima huku akitahadharisha
tabia inayojitokeza ya baadhi ya
wakulima wanaopata nyadhifa za
kisiasa, kusahau walikotoka na
kuanza kuwakandamiza wenzao.
Akawahimiza pia wakulima ili
kupanua uelewa wawe na hamasa
ya kujifunza mambo mapya kwa
kusoma magazeti na machapisho
mengine likiwemo jarida la wakulima
la Pambazuko (Sauti ya Wakulima)
linalochapishwa na MVIWATA.
Kwa upande wake mratibu wa
kikao hicho ambaye pia ni Afisa
Masoko wa MVIWATA Bw. Jimmy
Mongi aliwahimiza wakurugenzi hao
wa bodi, wawatumie wajumbe wenye
uzoefu walioko masoko ya jirani ili
kuwafundisha na kuwajengea uwezo
wajumbe wapya wanaochaguliwa.
“Tunaamini kuwa wajumbe
wa mwanzo kwenye bodi hizi,
walijengewa uwezo mkubwa kielimu
kwa kupelekwa ziara mbalimbali
za mafunzo, hivyo tunapofikiria
kupata mafunzo kwa wajumbe
wapya tuwafikirie kwanza hawa,
ni wenzetu watatupatia elimu
hiyo kwa gharama ndogo na pale
panapohitajika utaalamu zaidi ndipo
tuombe msaada wa MVIWATA ofisi
kuu,” alisema Bw. Mongi
Kwa
upande
wake
Bibi.
Honolata Blass, mjumbe wa bodi
ya Soko la Nyandira alisema bodi
za wakurugenzi zinapaswa kuwa
na ubunifu ili kuongeza ufanisi wa
masoko. “Kwa upande wetu ubunifu
wa bodi umesaidia kuongeza mapato
ya soko kila mwaka na kulifanya soko
kuwanufaisha wakulima wengi,”
alisema Bibi Blass.
Bodi hizo za wakurugenzi wa
masoko hukutana mara kwa mara
kwa lengo la kuwapa wadau hao
fursa ya kushirikishana uzoefu wa
mafanikio, changamoto na kuweka
mikakati ya uendelevu wa masoko
hayo ya wakulima.
Kikao
hiki
kilikutanisha
wakurugenzi 25 wa bodi za masoko
ya Kibaigwa wilaya ya Kongwa,
Nyandira wilayani Mvomero, Tandai
na Tawa Morogoro Vijijini, Mkata
wilaya ya Handeni na Igagala wilayani
Njombe.
Masoko hayo yalijengwa na
MVIWATA tangu mwaka 2004 na
kukabidhiwa kwa halmashauri za
wilaya na uendeshaji wake kubakia
mikononi mwa bodi za wakurugenzi
ambazo zinaundwa na wakulima na
wawakilishi wa halmashauri.
Kufunga mipaka ya kuuza mazao nje ya nchi
kunamsababishia hasara mkulima
Na Martin Pius, Babati
S
erikali imetakiwa kutotoa
amri za kuzuia mazao ya
chakula yakiwamo mahindi
kuuzwa nje ya nchi kwani kufanya
hivyo inawasababishia hasara
wakulima na kuwakatisha tamaa
ya kuongeza uzalishaji.
Rai hiyo imetolewa Julai
13, 2011 na Mjumbe wa Bodi
ya Mtandao wa Jinsia Tanzania
(TGNP), Bibi Rehema Mwateba
wakati akifungua Mkutano Mkuu
wa nne wa MVIWATA Manyara
uliowashirikisha wanachama wa
wilaya tano za mkoani Manyara.
Bibi Mwateba alisema Serikali
itambue kwamba inatumia mfumo
kandamizi kwa mkulima kwa kufunga
mipaka ya kuuza mazao ndani na nje
ya nchi bila ya kujali kuwa hilo ni
hitaji la mkulima la kuendesha maisha
yake yanayotegemea hasa bei nzuri
ya mazao. Alisema kuzuia biashara
ya mazao kwa kutumia kisingizio cha
kinga ya njaa hakitavumilika kwani
wakati utafika wakulima watachukua
hatua ambazo huenda zikawa na
madhara makubwa kwa taifa.
“Serikali inatakiwa kufanya
utafiti wa haraka kubaini maeneo
yaliyoathirika na njaa na kupeleka
chakula cha msaada na kwa maeneo
mengine yasiyokuwa na uhaba wa
chakula wakulima waruhusiwe
kuuza mazao yao nje ya nchi ili
kuweza kupata faida,” alisema.
Makamu
Mwenyekiti
wa
MVIWATA Manyara, Bibi Fatuma
Kimolo, akizungumza kwenye
mkutano huo alisema kama serikali
Endelea Uk wa 21
20
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
KUTOKA MITANDAONI
Wakulima washauriwa wasidai
posho za mafunzo
Na Ledis Kigala, Kyela
B
aadhi ya wakulima wilayani
Kyela
mkoani
Mbeya
wamewaasa
wenzao
kutanguliza mbele manufaa ya
elimu wanayopata katika kshiriki
kwao kwenye mafunzo badala ya
kudai posho.
Wamesema mtindo wa kudai
posho kwanza, unawafanya wakulima
kushindwa kupata elimu muhimu
kwa ustawi wa maisha yao.
Walitoa wito huo wakati wa
kufunga mafunzo ya kuwajengea
uwezo katika uzalishaji bora wa
mazao ya mpunga, mahindi, kokoa
na ufugaji wa wanyama.
Mmoja wa wakulima hao Bw.
Goden Mwantimwa wa kijiji cha
Lutusyo kata ya Muungano wilayani
Kyela alieleza kufurahishwa na
elimu na mafunzo yanayoendelea
kutolewa na Mtandao wa Vikundi
vya Wakulima Tanzania (MVIWATA)
na kuahidi kuwa ataendelea kushiriki
kwa sababu kwake elimu ni muhimu
kuliko posho.
“Mimi niko tayari kujitolea
kushiriki mafunzo mengine hata kama
itakuwa nje ya hapa, nawaombeni
wenzangu tuithamini sana elimu hii
ili itusaidie katika kuboresha kilimo
chetu,” alisema Bw. Mwantimwa.
Kwa upande wake Bw. Musa
Mwangongolo mkulima wa kijiji
cha Makwale kata ya Makwale,
alisema tabia ya kudai posho
kutoka kwa waandaaji wa mafunzo
imesababbisha wadau mbalimbali wa
maendeleo kuwakimbia wakulima
wa eneo hilo.
Alisema matokeo yake ni
waandaaji kuhamishia mafunzo hayo
katika maeneo mengine na kuwaacha
wakulima wa Kyela wakiwa hawana
la kufanya.
Alisema kimsingi wakulima siyo
masikini wa kipato, na kwamba
umasikini wao ni maarifa ambayo
MVIWATA imeonyesha njia ili
kufikia azma ya kuboresha kilimo ili
kiwe chenye tija zaidi.
Mafunzo hayo yaliyofanyika kuanzia
tarehe Septemba 21 hadi Oktoba 11,
2011 kwenye vijiji 18 vilivyoko kwenye
kata 10 za wilaya ya Kyela yalilenga
kuwapa elimu wakulima ya kuongeza
Bibi Edina Mwakipesile mkulima wa kijiji cha Mwiyonde wilayani Kyela akielezea dhana
ya MVIWATA kwa wakulima wenzake walioshiriki mafunzo ya kujengea uwezo vikundi,
yaliyoandaliwa na MVIWATA mjini Kyela.
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
uzalishaji pamoja na ubora wa mazao
na mifugo.
Mafunzo hayo ni sehemu ya
utekelezaji wa mradi wa Uhifadhi
Mazingira na Kukuza kipato
kwa wakulima wadogo waishio
kandokando ya ziwa Nyasa,
unaotekelezwa
na
MVIWATA
kwa ufadhili wa Shirika la Swedish
Cooperative Center (SCC).
Afisa Mradi huo Bw. Ledis Kigala,
alisema, mradi huo unatekelezwa
kwenye kata 10 kati ya kata 20
za wilaya ya Kyela ambazo ni
Bujonde, Ikolo, Ngonga, Ikimba,
Katumbasongwe, Ipande, Mwaya,
Ipinda, Muungano na Makwale.
Kufunga mipaka ya kuuza
mazao nje ya nchi...
Inatoka uk. wa 20
imeamua kufunga mipaka ya kuuza
chakula inatakiwa sasa ijipange
kununua mazao hayo ya wakulima
kwa bei yenye tija badala ya
kupanga bei yake isiyokuwa na
maslahi kwa mkulima.
Bibi Kimolo alisema kufungwa
mipaka kipindi hiki kumesababisha
bei ya mahindi kushuka kutoka
Sh. 45,000 na kufikia Sh 30,000
kwa gunia, hali ambayo inarudisha
nyuma maendeleo ya mkulima.
Alihoji kuwa iweje watumishi
wa
Serikali
wapandishiwe
mishahara kila mwaka kutokana
na kupanda kwa gharama ya
maisha, huku mkulima akiwekewa
masharti ya kupata ujira stahiki ili
aweze kukabiliana na hali ngumu ya
maisha magumu kwa kuuza mazao
kwenye soko lenye bei nzuri?
Alisema umefika wakati sasa,
serikali iache kutumia raslimali
nyingi kwenye kutoa na kusimamia
matamko ambayo hayana tija kwa
ustawi wa wakulima badala yake
nguvu na raslimali hizo zitumike
kuimarisha miundombinu ya
kilimo ili kiweze kuwa na uzalishaji
wa kutosheleza mahitaji ya chakula
na ziada ya biashara.
21
KATUNI
MUDA
MREFU NAONA
UNASOMA HILO
GAZETI LINA
HABARI GANI?
AH! GAZETI
LENYEWE LINA
HABARI ZA MJINI TU,
SIONI HATA HABARI
INAYOGUSIA KERO
ZETU.
OH! KWELI NDIO
SABABU
WAANDISHI
WENGI WANAJISHUGHULISHA NA
MAMBO YA MJINI
TU.
WEWE UTAZIPATA VIPI HABARI ZA
MJINI WAKATI GAZETI
LINACHUKUA SIKU 4
KUFIKA HAPA
AHA
HAHA SIO HIVYO,
NI MFUMO WA TAARIFA
YA MASOKO MVIWATA.
NAPATA TAARIFA KUPITIA SIMU YANGU YA
MKONONI TU.
22
SI
NINATUMIA
SIMU YANGU YA
MKONONI
ONA
SASA MIMI
SIJUI HATA KUTUMIA
HUO MTANDAO, HEBU
FIKIRIA NI WATU WANGAPI HAWAPATI HIZO
HABARI?
HIVI KWANINI SISI
WATU WA VIJIJNI
HABARI ZETU
HAZIANDIKWI?
NDIO MAANA
HAKUNA HABARI ZA
KILIMO KWENYE
MAGAZETI
MENGI!
NANI ATAKUJUA
HUKU KIJIJINI
AH!
MBONA
MWAKA JANA
WAANDISHI WALIKUJA WENGI TU
HUKU
HABARI ZITAFIKAJE
YAANI
UNAWAULIZA
WATU WA MJINI KWA
SIMU!?
LAKINI MIMI NAONA BADO
HIZO HABARI UNAZOPATA
KWENYE SIMU HAZIZUNGUMZII KILIMO
WE UMESAHAU!? SI KWA
SABABU WALILETWA
NA WAHESHIMIWA
KWENYE KAMPENI
LAKINI
MIMI NAPATA
TAARIFA NYINGI ZA
MASOKO YA MJINI
KILA SIKU.
HAPANA
NATUMIA
MTANDAO
MTANDAO
WA WAKULIMA
MVIWATA?
HAWA
WAANDISHI
WANAUPENDELEO
BWANA!
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
KATUNI
HUKU
HABARI ZA
KILIMO HAZIANDIKWI
NA WAKIANDIKA GAZETI
LINACHELEWA KUFIKA
AU LISIFIKE KABISA.
NDIO, BARABARA SIYO
NZURI KUWEZA KUSAFIRISHA MAGAZETI
YAFIKE HARAKA
LAKINI TUSIWALAUMU SANA
WAANDISHI, MIMI NAFIKIRI
SERIKALI YETU IANGALIE NA
MIUNDO MBINU YETU
SASA HUKU KWETU
BARABARA NI TATIZO
LABDA TUTAPATA HIZO
HABARI KWENYE RADIO NA TV
KWELI TUTAPATAJE
MAENDELEO KAMA HATUJUI
TAARIFA YA KILA SIKU YA
MASOKO, UCHUMI NA
SIASA?!
WATU WENGI WANAKUFA KWA KUKOSA
ELIMU YA AFYA NA KUAMINI IMANI POTOFU ZA KWENDA KWA WAGANGA.
ACHA UCHUMI
TU, IDADI KUBWA YA
WATANZANIA WANAISHI
VIJIJINI NA UMEME
HAKUNA HAYO MATANGAZO WATAYAONA
VIPI?
HATA KAMA ZIPO KUTOKANA NA HALI YA UCHUMI JE, TUTAWEZA KUNUNUA
HIZI TV NA UMEME
TUTAPATA WAPI?
HAPO
MAENDELEO
YATACHELEWA
SANA
WANAHABARI
WANA NAFASI KUBWA
SANA YA KUELIMISHA
WATU KUHUSU MATUMIZI
BORA YA ARDHI, UFUGAJI BORA, BEI KATIKA
MASOKO
EH
HAYO YOTE
YANATOKEA SABABU
HATUPATI HABARI
SAHIHI!
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
SASA
NAFIKIRI MUDA
MUAFAKA KWA WAHUSIKA KULIANGALIA HILI, SABABU VYOMBO
VYA HABARI NDIO VINAWEZA KUWAELIMISHA WATU NA KULETA
MAENDELEO HARAKA.
ITATUSAIDIA KUPATA ELIMU SAHIHI YA
AFYA, UKATILI DHIDI
YA WANAWAKE
HILI TATIZO LIFANYIWE KAZI, SABABU HATA RADIO ZENYEWE
HAZIFIKI VIJIJINI NA ZINATANGAZA UDHAIFU TU WA WATU WA
KIJIJINI INGAWA KUNA MAFANIKIO NA UBUNIFU WANAOUFANYA.
Kwaherini
KWELI
BARABARA NI
TATIZO KWA SABABU
HATA MTOTO WA MZEE
KIPARA ALIFARIKI KWENYE
GARI KWA UBOVU WA
BARABARA.
JUZI NILIKUWA MJINI
NIMEONA MATANGAZO MENGI
YANAYOONESHA UDHAIFU
WA WATU WA KIJIJINI TU
INA MAANA HUKU HATUNA
MAMBO MAZURI YA KUTANGAZA NA TV?
wasalimie rafiki
zangu’
23
KUTOKA MITANDAONI
Mfumo shirikishi unaharakisha
maendeleo
Na Gratian Cronery, MUCCoBS
Shinyanga
M
aendeleo
na
ustawi
wa miradi ya kijamii
yanategemea
zaidi
ushirikishwaji wa jamii husika
katika hatua zote.
Katika nchi yetu hali ni
tofauti ambapo miradi mingi
wanayopelekewa
wananchi
hawakushirikishwa kikamilifu na
kwamba kinachofanyika ni wao
kupokea amri ya bwana mkubwa na
kutekeleza wasichokijua.
Hali
hii
ya
kuwapelekea
wananchi maamuzi badala ya wao
kushiriki kuibua wazo na kuamua,
imesababisha miradi mingi kutotoa
matokeo chanya licha ya kugharimu
fedha nyingi.
Serikali
katika
kuwasaidia
wananchi kutekeleza mipango ya
maendeleo imekuwa ikianzisha
miradi ikiwemo ya kujenga majengo
kwa lengo la kuwasaidia wananchi, ila
ukweli ni kwamba fedha na raslimali
nyingi zimekuwa zikipotea bure.
Iko mifano mingi ya miradi ya
aina hii ambayo wananchi wanaipa
jina la ‘miradi ya serikali’ kwa kuwa
hawakushirikishwa na haikuwa
kipaumbele chao. Miradi hii ni kama
vile ya majengo ya masoko kwenye
vijiji vya Ruvu Darajani mkoani
Pwani, Buigiri wilaya ya Chamwino,
Ruaha mkoa wa Iringa na kwingineko
ambayo yametelekezwa na kuwa
vichaka vya wezi ama nyumba ya
wanyama na wadudu, baada ya
wananchi kususa kuyatumia kwa
kuwa haikuwa kipaumbele chao
na kwingineko uchaguzi wa eneo
haukuwa sahihi.
Huu ni mmoja wa mifano ya
24
miradi mingi ambayo imeanzishwa
na serikali pasipo kuwashirikisha
wananchi katika kutoa mawazo yao
na kupendekeza nini wanahitaji na ni
kwa matumizi gani, na kama ni jengo
likae sehemu gani.
Mfumo uliotumika kuanzisha
na kutekeleza kauli mbiu ya “kilimo
kwanza” ni ule ule wa amri kutoka
kwa bwana mkubwa, mkulima hana
hiari cha kuchagua kukataa hata
kama kilicholetwa ni mwiba kwake.
Vile vile serikali imekuja na
mpango wa zana bora za kilimo
ikiwemo matrekta madogo (power
tiller) na ambapo kwenye maeneo
mengi hazihitajiki kutokana na
aina ya udongo na mazingira.
Baada ya wakulima kulazimishwa
kuzinunua wamezigeuza matumizi
na kuwa mashine za kufua umeme,
kusukuma maji, kulanda mbao na
kusaga unga.
Hii ni changamoto kwa serikali na
wadau wengine ambao wanatazamia
kupeleka miradi kwa wananchi,
kwamba ni vyema kuzingatia
ushirikishwaji wa wananchi na
mawazo
yao
yakaheshimiwa
ili
baadaye
wakithamini
wanachopelekewa.
Watanzania wanakabiliwa na kero
nyingi ambazo wangetarajia serikali
kuwekeza nguvu zake zaidi kwa
kutumia mfumo wa ushirikishwaji
katika kuzitatua. Kwa mfano
kuondoa kero ya ushuru mkubwa
wa mazao unaotozwa kwenye
vizuizi vya kila barabara ya nchi hii
inayoelekea mjini. Kuna maana gani
kumpa ruzuku ya pembejeo mkulima
na baadaye kumkamua faida yote
inayotokana na mavuno hayo?
Kama ushuru unatozwa ili kufidia
fedha za ruzuku, ni bora ruzuku
hiyo ifutwe wakulima wajitafutie
pembejeo na wawe huru kusafirisha
mazao yao. Hili linaweza kutatuliwa
kwa njia shirikishi ya majadiliano.
Kwa kufanya hivyo tunaweza
kutengeneza mipango na miradi
endelevu kwa vizazi na vizazi ambayo
italeta tija katika nyanja zote za
maisha kisiasa, kiuchumi na kijamii.
Kwa upande mwingine tumeona
mfano wa miradi ya ujenzi wa masoko
inayotekelezwa na MVIWATA
kwa mfumo shirikishi imefanya
vyema na wakulima wanathibitisha
matokeo yake. Mwenyekiti wa
MVIWATA Shinyanga Bw. Charles
Ndugulile anasema siri kubwa ya
mafanikio ya masoko ya MVIWATA
ni kuzingatiwa kwa dhana ya
ushirikishwaji.
“MVIWATA imefanikiwa kufanya
hivyo kwa hutoa mafunzo mazuri
ya jinsi ya kushirikisha jamii kuanzia
ngazi ya kaya hadi taifa ambayo
huambatana na mafunzo ya andiko
la mradi, uendeshaji na usimamizi
wa miradi, uhasibu wa vikundi na
mashirika pamoja na taasisi pamoja
na mifumo ya masoko na biashara,”
anasema Bw. Ndugulile.
Endapo serikali na wadau
wengine wa maendeleo watatumia
dhana hii ya ushirikishwaji wa jamii
kwa mapana na kuiona kama fursa
ya kuleta mabadiliko chanya kwa
jamii ya Watanzania, hakika taifa
litapiga hatua ya ukuaji wa kasi wa
maendeleo.
Jamii kwa upande wao pia
wanapaswa
kujipanga
vyema
kushiriki katika mradi kwa kuibua
wazo, kupanga, kutekeleza na
kusimamia na baadaye kujipima
kiwango cha uwajibikaji wao kwenye
miradi husika.
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
MAWAKALA
Jipatie nakala ya Jarida la Pambazuko katika ofisi
za MVIWATA ngazi za kati zifuatazo
Mratibu
MVIWATA Morogoro
S.L.P 3220 Morogoro
Mahali: Uwanja wa Maonyesho NaneNane mkabala na
ofisi za TASO
Simu/Faksi: 023 261 41 84
Barua Pepe: [email protected]
Mratibu
MVIWATA Rukwa
S.L.P 468 Sumbawanga
Mahali: Jengo la Bethlehem Center – Barabara ya Msakila
Faksi: +255 25 280 25 58
Simu: +255 764 232 747, +255 784 940 606
Barua pepe: [email protected]
Mratibu
MVIWATA Mbeya
S.L.P 3015 Mbeya
Mahali: Jengo la Bima na CRDB Bank (Ghorofa ya
mwisho
Simu: +255 784 979 397, +255 652 835 568
Barua pepe: [email protected]
Mratibu
MVIWATA Chunya
Mahali: Jengo la Halmashauri, chumba Na.3
Barua pepe: [email protected]
Mratibu
MVIWATA Iringa
S.L.P 918 Njombe
Mahali: Jengo la Njoluma, Njombe mjini
Simu: 0782 241 224, +255 767 241 224
Barua pepe: [email protected]
Mratibu
MVIWATA Kilimanjaro
S.L.P 7389 Moshi
Mahali: Mbuyuni sokoni- ghorofa ya GOLDEN GROWN
LODGE
Simu: +255 27 275 16 39, +255 784 720 320
Barua pepe: [email protected]
Mratibu
MVIWATA Kagera
S.L.P 1753 Bukoba Mjini
Mahali: Ofisi za Mayawa-Mtaa wa Rwamishenyi, Barabara
ya Uganda
Simu: +255 788 685818, +255 782 154961, +255 755 522 447
Barua pepe: [email protected]
Mratibu
MVIWATA Dodoma
S.L.P 3293 Dodoma
Mahali:Area C Dodoma eneo la INADES Formation
Tz,mkabala na msikiti wa Area C
Simu:255-26-2350013, +255 782 257 783,
+255 767 881 352
Faksi: +255 26 2350744
Barua pepe: [email protected]
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
Mwenyekiti
MVIWATA Monduli (MVIWAMO)
S.L.P 47 Monduli
Mahali: Barabara ya Boma-Moringe Sekondari, Monduli
Mjini
Simu: 255-27-253 8029, +255 27 253 8337
Faksi: +255 27 253 8338
Barua pepe: [email protected]
Mratibu
MVIWATA Manyara
S. L. P. 446,
Babati Manyara
Mahali: Barabara ya Nyerere
SIMU: +255 27 253 0385 Faksi: +255 27 253 0707
Baruapepe: [email protected]
Mwenyekiti
MVIWATA Tabora
S.L.P 175 Igunga
Mahali: Mtaa wa Uarabuni
Simu: +255 784 398 414, +255 782 219 551
Barua pepe: [email protected]
Mratibu
MVIWATA Zanzibar
S.L.P 149 Zanzibar
Mahali: Mwana kwerekwe- mkabala na shule ya sekondari
M’kwerekwe A
Simu: +255 773 926 955, +255 777 470 518
+255 783 651 135
Barua pepe: [email protected]
Mratibu
MVIWATA Ruvuma
S.L.P 696 Songea Manispaa
Mahali: Jengo la TTCL ghorofa ya 2
Simu: +255-25-2600626, +255 756 096 291
Barua pepe: [email protected]
Mratibu
MVIWATA Mkuranga
S.L.P 56 Mkuranga
Mahali: Karibu na Stendi ya Kimanzichana
Simu: 0786 158 646
Barua pepe: [email protected]
Mwenyekiti:
MVIWATA Shinyanga
S.L.P 1024 Shinyanga
Mahali: Chuo cha Ushirika Moshi tawi la Shinyanga
(Kizumbi)
Simu: +255 763 740 675, +255 755 546 311
Barua Pepe: [email protected]
Mwenyekiti
MVIWATA Kigoma
S.L.P 1144 Kigoma
Mahali: Ndani ya ofisi ya KIKANGONET, Lumumba road
jengo la NHC chumba 205
Simu: 0713 565 252, 0762 565 252
Barua pepe: [email protected]
25
IJUE MVIWATA
Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania- MVIWATA
Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA) ni chombo cha kuunganisha wakulima wadogo ili kuwa na sauti moja katika utetezi wa
maslahi yao ya kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na kisiasa.
Mtandao huu ulianzishwa mwaka 1993 na wakulima wadogo. Kauli mbiu ya MVIWATA ni ‘Mtetezi wa Mkulima ni Mkulima
Mwenyewe’.
Falsafa, utume na dira ya MVIWATA
Falsafa ya MVIWATA inajengwa katika ya misingi ya ushawishi na utetezi wa maendeleo ya wakulima wadogo katika nyanja za kiuchumi na
kijamii; kuwezesha mawasiliano na kujifunza kwa kubadilishana uzoefu miongoni mwa wakulima.
Utume wetu:
Kuimarisha mawasiliano na kuwaunganisha wakulima wadogo kupitia vikundi na mitandao yao katika ngazi mbali mbali ili kujenga mtandao wa
kitaifa wenye nguvu ya kuwezesha ushiriki na uwakilishi wa kweli wa maslahi ya wakulima wadogo katika ngazi zote za maamuzi.
Dira yetu:
MVIWATA ni kuwa chombo imara chenye nguvu za ushiriki na uwakilishi wa mawazo ya mkulima katika mchakato wa maamuzi ya kiuchumi,
kijamii na kisiasa. Kuwa na uwezo wa kutekeleza na kufuatilia michakato na shughuli za maendeleo ya kiuchumi na kijamii yanayogusa maslahi ya
wakulima wadogo.
Malengo ya MVIWATA
1. Kuwezesha mawasiliano miongoni mwa wakulima wadogo ili kujenga kwa pamoja mbinu na mikakati ya ushawishi na utetezi kwa maslahi ya
wakulima wadogo, kiuchumi na kijamii.
2. Kubadilishana mawazo, ujuzi na uzoefu juu ya kilimo na shughuli mbalimbali za wakulima ili kuboresha maisha na kuinua hali yao kiuchumi na
kijamii.
3. Kuwakilisha wakulima wadogo katika mashauriano na serikali juu ya masuala mbalimbali yanayohusu au yanayoathiri ufanisi na maslahi ya
wakulima wadogo wa Tanzania.
Maeneo makuu ya mpango mkakati
1. Ushawishi na Utetezi: Kuwezesha wakulima wadogo kuwa na uwezo wa kutetea maslahi yao.
2. Uwezo wa kiuchumi: kuwezesha wakulima wadogo kuwa na uwezo wa kiuchumi kupitia njia za akiba na mikopo, kuunganisha wakulima na
masoko na elimu ya ujasiliamali
3. Kuimarisha vikundi na mitandao ya wakulima kwa lengo la kujipanga na kujitetea.
4. Masuala mtambuka: Kujenga uelewa wa wakulima juu ya Ukimwi, Jinsia, Mabadiliko ya Tabia ya nchi.
5. Ujenzi wa kitaaasisi kwa lengo la kuimarisha shirika
Muundo
Muundo wa MVIWATA una ngazi tatu ambazo ni Ngazi ya Taifa, Ngazi ya Kati na Ngazi ya Msingi. Ngazi ya Kati inaundwa na mitandao ya
kimkoa na kiwilaya wakati Ngazi ya Msingi inaundwa na mitandao ya Kata na Vijiji.
Shughuli kuu
1. Kujenga uwezo wa wakulima wadogo kwa kupitia mafunzo shirikishi juu ya mbinu za ushawishi na utetezi, mbinu za kuimarisha uchumi wa
wakulima wadogo na uendelevu wa rasilimali kwa njia za warsha, mafunzo, mikutano na ziara za mafunzo.
2. Kuhamasisha wakulima wadogo kujiunga katika vikundi vya kijamii na kiuchumi, mitandao ya msingi (kata na vijiji) na mitandao ya kati (mikoa
na wilaya). Mpaka sasa MVIWATA imeanzisha mitandao ya kimkoa katika Mikoa ya Dodoma, Iringa, Kagera, Kilimanjaro, Manyara, Mbeya,
Morogoro, Rukwa, Ruvuma, Shinyanga, Tabora na Tanga kwa Tanzania Bara. MVIWATA pia imeanzisha mitandao ya kiwilaya katika Wilaya
za Monduli (Arusha) na Chunya (Mbeya). Tanzania Visiwani, MVIWATA Zanzibar imeanzishwa na kusajiliwa (Usajili namba 401). Mkakati
unaendelea wa kuimarisha mitandao iliyopo na kuanzisha mitandao mipya.
3. Kukusanya, kuweka katika kumbukumbu na kusambaza habari zinazohusu ujuzi na uzoefu wa wakulima, sera za kitaifa na kimataifa kwa
kupitia jarida la Pambazuko Sauti ya Wakulima, vipindi vya radio, vipeperushi, vijitabu na machapisho mengine.
4. Kuhamasisha na kuwezesha wakulima kubuni na kuendesha miradi shirikishi ya kiuchumi na uzalishaji kwa lengo la kuboresha uchumi wa
wakulima wadogo kama vile vyama vya mazao, vyama vya kuweka na kukopa na masoko ya mazao.
5. Kuandaa mikutano na warsha kuhusiana na mada zinazowagusa au kuathiri maslahi ya wakulima wadogo.
Uanachama na jinsi ya kujiunga na shirika
MVIWATA ina wanachama wa aina tatu (3).
Aina ya kwanza ni Wanachama wa Kawaida ambao wamegawanyika katika makundi mawili;
a) Kikundi cha wakulima wadogo au
b) Mkulima mdogo binafsi aliye mwanachama katika Kikundi au Mtandao. Mkulima atakuwa mwanachama wa kawaida wa MVIWATA mara
tu Kikundi au Mtandao wake utakapokubaliwa kuwa mwanachama. Atapewa kadi ya uanachama na kikundi au mtandao utapewa cheti cha
utambulisho.
Aina ya pili ni Vyama, Mashirika na Mitandao ya Wakulima Wadogo.
Vyama, Mashirika na Mitandao ya Wakulima Wadogo vinavyojishughulisha na utetezi na ushawishi wa maslahi ya wakulima wadogo vilivyosajiliwa
chini ya sheria yoyote ya Tanzania katika Ngazi za Wilaya, Mkoa au Taifa vinaweza kuomba kuwa mwanachama wa MVIWATA iwapo vinakubaliana
kwa dhati na malengo na madhumuni ya Shirika.
Aina ya tatu ni Wanachama Washiriki
Ni mtu yeyote, taasisi au kikundi cha watu ambacho kinaunga mkono malengo na madhumuni ya Shirika. Mwanachama mshiriki anatamkwa na
Mkutano Mkuu wa MVIWATA.
Kila mwanachama, isipokuwa mwanachama mshiriki atalipa kiingilio na ada ya kila mwaka. Maelezo zaidi juu ya utaratibu wa kujiunga na ada
yanapatikana kutoka kwa kiongozi au ofisi ya MVIWATA.
Kwa mawasiliano zaidi
Ofisi Kuu ya MVIWATA
Mkurugenzi Mtendaji
MVIWATA
S.L.P 3220 Morogoro
Simu: 023 261 41 84
Faksi: 023 261 41 84
Barua pepe: [email protected], [email protected]