de pita tangas

Transcription

de pita tangas
THE UNITED NATIONS CHILDREN'S FUND – UNICEF
TANZANIA
KIVUNGE CHA MKAKATI WA MAWASILIANO KATIKA
KUKABILIANA NA MAAFA
FEBRUARI, 2013
YALIYOMO
DIBAJI ...................................................................................................................................................... 1
WILAYA YA MAGHARIBI, UNGUJA- MAFURIKO ........................................................................ 16
WILAYA YA KINONDONI, DAR ES SALAAM-MAFURIKO ......................................................... 24
WILAYA YA HANDENI, TANGA-MLIPUKO WA KIPINDUPINDU .............................................. 28
WILAYA YA KILOSA, MOROGORO-MAFURIKO .......................................................................... 32
WILAYA YA MICHEWENI, PEMBA-UKAME.................................................................................. 36
WILAYA YA KINONDONI, DAR ES SALAAM-MAFURIKO ......................................................... 40
WILAYA YA LONGIDO, ARUSHA-UKAME .................................................................................... 44
WILAYA YA MAGHARIBI, UNGUJA-MAFURIKO ......................................................................... 48
KIAMBATANISHO No 1: UJUMBE MHIMU NA NJIA ZA MAWASILIANO ZINAZOTUMIKA
KWA SASA NA NJIA MPYA ZILIZOPENDEKEZWA KUTUMIKA ................................................... 51
ii
DIBAJI
Kivunge hiki kimetayarishwa kutokana na mkakati wa mawasiliano wa kukabiliana na maafa
uliotayarishwa kwa ajili ya wilaya sita ambazo ni Micheweni, Pemba (Ukame), Magharibi
Unguja (Mafuriko), Longido, Arusha (Ukame), Handeni, Tanga (Milipuko ya kipindu pindu),
Kilosa, Morogoro (Mafuriko) na Kinondoni, Dar es Salaam (Mafuriko).
Kivunge hiki kimetayarishwa ili kusaidia kupashana habari muhimu na walengwa ambao wengi
wao ni waathirika wa ukame, mafuriko na milipuko ya magonjwa ya kipindupindu kabla, wakati
na baada ya majanga hayo kutokea.
Kivunge hiki pia kinatoa taarifa ambazo zinaweza kutumiwa moja kwa moja na walengwa
ambazo zitaweza kuwasilishwa kupitia njia mabali mbali za mawasiliano kama vile Redio,
Televisheni, mtandao wa intaneti, simu za mkononi, magazeti, vipeperushi na posta ambazo
zinaweza kuwekwa kwenye mabango makubwa.
Kivunge hiki kina jumla ya skripti (script) 24, kila skripti inabeba ujumbe mhimu ambao
unaweza kuwasilishwa na kuwafikia walengwa kwa njia ya Redio na Televisheni.
Kivunge hiki pia kimesheheni vikaragosi (Cartoons) 24 ambavyo vimeandaliwa kufikisha
ujumbe kwenye wilaya zote sita. Kivunge hiki kimeandaliwa kwa lugha ya Kiswahili ili kuweza
kuwafikia walengwa wengi kwa urahisi.
1
WILAYA YA HANDENI, TANGA – MILIPUKO YA KIPINDUPINDU
TANGAZO LA REDIO 1
WAHUSIKA
:
SAMBONI NA LUKA
MAHALI
:
KIBANDA CHA CHIPS/BAR
SAUTI NA MILIO
:
HONI NA NGURUMO ZA MAGARI NA KELELE ZA
WATU
1. SEKIMWEI
:
Hizo Chips vipi?
2. SAUTI NA MILIO
:
MTU AKINAWA MIKONO
3. SEKIMWEI
:
Wewe mbona haya maji baridi?
4. LUKA
:
Kwani yana tatizo gani?, nawa mzee nina wateja wengine
wananisubiri.
5. SEKIMWEI
:
Wewe mgonjwa nini? Unataka kutuua wenzio na
kipindupindu.
Hao wateja wote watakuwa hawaji hapa kwako kama
wataugua
Kipindupindu na magonjwa ya kuhara.
6. LUKA
:
Mzee unanizingua bwana. Hii biashara bwana! Maji ya
kunawa ya moto nyumbani kwako.
7. SEKIMWEI
:
Unasemaje? Wewe mjinga tunatakiwa kunawa mikono
kwa maji
ya moto na sabuni kabla ya kula ili kuua vijidudu vya
Kipindupindu na magonjwa ya kuhara,…lazima ujue kijana
wangu la sivyo Kipindupindu hakitakoma hapa kwetu au
naongea uongo ndugu zangu?
8. WATU
:
Uko sawa kabisa mzee mwenzetu.
2
TANGAZO LA REDIO 2
WAHUSIKA
:
SEKIDIA NA MA’ MHANDO
MAHALI
:
KWA SEKIDIA
SAUTI NA MILIO :
MILIO YA KUKU NA MBUZI
1. MA’MHANDO :
Shemeji uani ni wapi? Naona tumbo haliko vizuri.
2. SEKIDIA
Subiri kidogo shemeji nakuja
:
3. SAUTI NA MILIO:
MLANGO UNAFUNGULIWA.
4. MA’MHANDO :
Haaaaa!!! Shemeji unanipa jembe maana yake nini?
5. SEKIDIA
Zunguka hapo nyuma kwenye migomba kule, chimba
:
jisaidie huko utuwekee mbolea. Hatujachimba choo
shemeji……. wenyewe tumezoea. Watu wote huku
wanajisaidia porini.
6. MA’MHANDO :
Shemeji….shemeji haaaaa, karne hii ya digitali bado
mnajisaidia porini…… aaaaah ndio maana huku kwenu
Kipindupindu na Magonjwa ya Kuhara hayaishi, Shemeji
Sekidia… ili muweze kuepukana na milipuko ya Kipindu
pindu ni kutumia choo… Kipindupindu husambaa kwa
haraka kupitia uchafu na vinyesi. Shemeji
chimba choo, hii ni hatari kwa usalama wa maisha yenu.
7. SEKIDIA
:
8. MA’MHANDO :
Nimekusikia Shemeji yangu, nitalifanyia kazi
Choo ni muhimu sana kwa maisha yenu, siondoki mpaka
nihakikishe umechimba choo, uwe mfano kwa wana jamii
wenzio.
3
TANGAZO LA TELEVISHENI
1
NJE : KIBANDA CHA CHIPS : JIONI : MJI :
Kinaonekana Kibanda cha Chips, wanaonekana watu kadhaa wakiwa wamekaa wanakula Chips,
mishikaki na Kuku. Mmoja wapo wa watu hawa ni mzee Samboni, amekaa akionekana akiwa
anasubiri huduma, anaonekana Kijana muuza Chips Luka akimletea Chips Mayai na Mishikaki
Miwili, anaweka sahani kwenye Meza na kuanza kumnawisha.
SAMBONI
Wewe mbona haya maji Baridi
LUKA
Kwani yana tatizo gani, nawa mzee nina wateja wengine
Wananisubiri.
SAMBONI
Wewe mgonjwa nini? Unataka kutuua wenzio na kipindupindu.
Hao wateja wote watakuwa hawaji hapa kwako kama wataugua
Kipindupindu na magonjwa ya kuhara.
LUKA
Mzee unanizingua bwana. Hii Biashara bwana.
SAMBONI
Tunatakiwa kunawa mikono kwa maji moto na sabuni kabla ya
kula ili kuua vijidudu vya Kipindupindu na magonjwa ya kuhara,
lazima ujue kijana wangu la sivyo Kipindupindu hakitakoma hapa
kwetu au naongea uongo ndugu zangu?
Anawaangalia wateja wengine huku na wenyewe wanaonekana kukubaliana nao, Luka nae
anaonekana kukubaliana na Mzee Samboni.
4
TANGAZO LA TELEVISHENI 2
NJE : JIONI : MBELE YA NYUMBA YA SEKIDIA : MTAANI : KIJIJINI :
Inaonekana Nyumba ya kawaida tu ya udongo lakini imepigwa Lipu, anaonekana mama Mhando
akiwa anaongea na Mzee Sekidia, anaonekana mama Mhando akisimama,
MAMA MHANDO
Shemeji uani ni wapi? Naona tumbo haliko vizuri.
SEKIDIA
Subiri kidogo shemeji nakuja
Anaonekena Sekidia akiingia ndani, Kisha anatoka akiwa na Jembe mkononi na kopo la
maji, Mama Mhando anaonekana Kushangaa.
SEKIDIA
Zunguka hapo nyuma kwenye migomba kule, chimba.
Hatujachimba choo. Wenyewe tumezoea.
MAMA MHANDO
Shemeji….shemeji haaaaa, karne hii ya Digitali bado
Mnajisaidia porini…… aaaaah ndio maana huku kwenu
Kipindupindu na Magonjwa ya Kuhara hayaishi, Shemeji
Sekidia… ili muweze kuepukana na milipuko ya Kipindu
pindu ni kutumia choo… Kipindupindu husambaa kwa
nguvu na haraka kwa kupitia uchafu na vinyesi. Shemeji
chimba choo, hii ni hatari kwa usalama wa maisha yenu.
SEKIDIA
Nimekusikia Shemeji yangu.
5
WILAYA YA MICHEWENI, PEMBA – UKAME
TANGAZO LA REDIO 1
WAHUSIKA
:
MWINCHANDE NA KIDAU
MAHALI
:
SHAMBANI
SAUTI NA MILIO :
SAUTI ZA NDEGE NA WADUDU
1. SAUTI NA MILIO:
MLIO WA PANGA AU SHOKA LIKIKATA MTI
2. KIDAU
We Mwinchande weye … mzima kweli weye?
:
3. MWINCHANDE :
Kwani vipi? Waniona natakiwa pelekwa kwa Dokta au
kwa Fundi.
4. KIDAU
:
Yaani weye ukame wote huu bado wakata mti, wenzio twasisitiza
watu wapande miti mpaka kwenye majumba yao wewe wakata,
mtumeeee…. Halafu mwembee wazaa huu !
5. MWINCHANDE :
Huu mti ni wangu, nimechoka fukuzana na watoto na watu wazima
wanaokuja niibia embe zangu, bora niukate tuu…mwenbe wangu
lakini wanao faidi wengine.
6. KIDAU
:
Huo ni uamuzi wa kitoto…..
7. MWINCHANDE:
Kwa hiyo waamua ntukana sasa? Si ndiyo?
8. KIDAU
Wala sikutukani, ila ntaka nikuambie, ili kuepukana na ukame
:
twatakiwa panda miti kwa wingi, hata mpaka kwenye maeneo
ya majumba yetu, tupande miti kila mahala….. acha hasira
weye. Au wewe huoni ukame huu.
9. MWINCHANDE :
Nauona, ni kweli jua la waka, basi nauacha, ahsante sana Bwana
Kidau.
6
TANGAZO LA REDIO 2
WAHUSIKA
:
MAMA JUMBE NA MAMA CHANDE
MAHALI
:
KWA MAMA JUMBE
SAUTI NA MILIO :
SAUTI ZA KUKU
1. MA’CHANDE
:
Hodi hapa…… za hapa?
2. MA’JUMBE
:
Hapa kwema, haya mwanamke weye na kikapu watokea
wapi?
3. MA’ CHANDE :
Natokea hapo kwa duka la pembejeo natoka nunua mbegu
za mahindi, kesho nipande.
4. MA’JUMBE
:
Na ukame huu bado tu unapanda mahindi, unachekesha.
5. MA’CHANDE
:
Sasa wewe ulitaka nipande nini? miwa?
6. MA’JUMBE
:
Mazao yanayovumilia ukame mwanamke wewe, si unaona
mwenzio hapa, nina mtama hapa na pale nina mihogo,
haya mazao yanavumilia ukame, kwa hali kama hii ni
vizuri tupande mazao yanayo himili ukame.
7. MA’CHANDE
:
Mmmmh!!! Lakini kweli maana hali si hali, jua kali kama
nini sijui, lakini tutakula nini sasa mihogo tu na mtama?
7
TANGAZO LA TELEVISHENI 1
NJE : ASUBUHI : SHAMBANI :
Aaonekana Bwana Mwinchande akiwa na Panga lake mkononi akiwa Shambani kwake akikata
Mti mkubwa wa mwenbe, anaonekana Bwana Kidau akiwa anapita mkononi na yeye akiwa na
Panga na kiroba kimekunjwa kunjwa, anasimama na kushangaa, anasogea
kabisa alipo
Mwinchande,
KIDAU
We Mwinchande mzima kweli weye?
MWINCHANDE
Kwani vipi? Waniona natakiwa pelekwa kwa Dokta au
kwa Fundi
KIDAU
Yaani weye ukame wote huu bado wakata mti, wenzio
twasisitiza watu wapande miti mpaka kwenye majumba
yao wewe wakata, mtumeeee.
MWINCHANDE
Huu mti ni wangu, nimechoka fukuzana na watoto na watu
wazima wanaokuja niibia Embe zangu, bora niukate tuu…
mwenbe wangu lakini wanao faidi wengine.
KIDAU
Huo ni uamuzi wa kitoto…..
MWINCHANDE
Kwa hiyo waamua ntukana sasa?
KIDAU
Wala sikutukani, ila ntaka nikuambie, ili kuepukana na ukame
twatakiwa panda miti kwa wingi, hata mpaka kwenye maeneo
ya majumba yetu, tupande miti kila mahala….. acha hasira
weye. Au wewe huoni ukame huu.
MWINCHANDE
Nauona, basi nauacha, ahsante sana bwana Kidau.
8
TANGAZO LA TELEVISHENI 2
NJE : JIONI : KANDO YA NYUMBA :
Ni nyumbani kwa Mama Jumbe, anaonekana amekaa kwenye kivuli cha nyumba, anapeta
Mtama, kwa kando yake kunaonekana lundo la miti ya Mihogo, ikiwa imekatwa katwa vipande,
anaonekana Mama Chande akiwa anaelekea alipo kaa Mama Jumbe, akiwa na kikapu mkononi.
MAMA JUMBE
Haya mwanamke weye na kikapu watokea wapi?
MAMA CHANDE
Natokea hapo kwa duka la pembejeo natoka nunua
mbegu za Mahindi, kesho nipande.
MAMA JUMBE
Na ukame huu bado tu unapanda mahindi, unachekesha.
MAMA CHANDE
Sasa wewe ulitaka nipande nini?
MAMA JUMBE
Mazao yanayovumilia ukame mwanamke wewe, si
unaona mwenzio hapa, nina mtama hapa na pale
nina mihogo, haya mazao yanavumilia ukame, kwa
hali kama hii ni vizuri tupande mazao yanayo himili
ukame.
9
WILAYA KILOSA, MOROGORO – MAFURIKO
TANGAZO LA REDIO 1
WAHUSIKA
:
MAMA MKUDE, WATU NA MTU 1
MAHALI
:
MKUTANONI
SAUTI NA MILIO
:
KELELE ZA WATU
1. MWENYEKITI WA KIJIJI
:
Tusikilizane jamani, tumeitisha mkutano huu ili
tuweze kuzungumzia athari za mafuriko katika
eneo letu na hapa tunaye kiongozi kutoka wilayani.
2. MA’MKUDE(Afisa Tawala Wilaya): Jamani tunaomba sana ushirikiano wenu, bila
nyinyi sisi serikali tutakuwa tunafanya kazi bure,
ndugu zangu Mjenga nchi………..
3. WATU
:
Ni Mwananchi
4. MA’MKUDE
:
Na mvunja nchiiiiiiiiiiii!!!!!!!
5. WATU
:
Ni huyo huyo Mwananchi
6. SAUTI NA MILIO
:
WATU WANAPIGA MAKOFI NA
VIGELEGELE
7. MA’MKUDE
:
Jamani tunawaomba sana acheni kulima kankando
ya mto Mkondoa, acheni kuchungia mifugo yenu
kando ya mto Mkondoa, hayo yote yana sababisha
mmomonyoko wa udongo na hatimae
husababisha mafuriko.
8. MTU 1
:
(KWA KUROPOKA) Sasa unataka tulime wapi na
kuchungia wapi wakati yale ndio maeneo yenye
rutuba na majani mazuri!
9. MA’MKUDE
:
Jamani sikilizeni maeneo ya Kulima na
kuchungia yapo mengi sana. Sasa nasema hivi
atakaye kwenda kinyume na amri hii akikamatwa
sheria itachukua mkondo wake, tumetunga sheria
ngumu ili tuweze kuulinda mto wetu.
Tumechoshwa na mafuriko katika Wilaya yetu;
10
tukiachia tabia hii iendelee ni sawa na kulipa dudu
liumalo…………
10. WATU
:
Kidole
11. MA’MKUDE
:
Si ndio jamani………..?
12. HADHARA
:
Ndiooooooooooooooooooooo!!!
11
TANGAZO LA REDIO 2
WAHUSIKA
:
SEKULU, MLOKA NA MAMA MLOKA
MAHALI
:
KWA SEKULU
SAUTI NA MILIO :
MBUZI NA KUKU
1. SEKULU
:
Mloka na Shemeji Ahsanteni sana kwa ushauri wenu.
2. MLOKA
:
Tunakushauri mengi Sekulu lipi hasa unalotushukuru?
3. SEKULU
:
Hili mliloniambia kwamba kusombewa vitu na mafuriko sio
mwisho wa maisha, nikakakope kamkopo kadogo, imenisaidia
nyumba ndio hii na biashara zangu zinaendelea vizuri maana
mafuriko ya mto Mkondoa yalinisombea kila kitu.
4. MA’MLOKA
:
Umeamini sasa Shemeji kukumbwa na mafuriko, sio mwisho
wa maisha.
5. SEKULU
:
Ni kweli, Shemeji…. Binadamu hutakiwi kukata tama, na mimi
nitawashauri wenzangu wakikutwa na hali kama yangu ya
kukumbwa na mafuriko wasikate tama, maisha yanatakiwa
kuendelea……….kukatika kwa koleo sio mwisho wa…………..
6. MLOKA NA MAMA MLOKA: Uhunzi………..
12
TANGAZO LA TELEVISHENI 1
NDANI : JIONI :UWANJANI : CHINI YA MTI : SHULENI MKUTANO
Ni mkutano mkubwa wa watu, wanaonekana Wake kwa Waume wakiwa katika Mavazi ya
aina Mbalimbali. Mbele yao anaonekana Mwanamama mmoja akiwa amesimama
jukwaani akiwa ana hutubia, huyu ni Mama Mkude, ni Afisa Tawala wa Wilaya………….
MAMA MKUDE
Jamani tunaomaba sana ushirikiano wenu, bila nyinyi
Sisi serikali tutakuwa tunafanya kazi bure, ndugu zangu
mjenga nchi
WATU WOTE
Ni Mwananchi
MAMA MKUDE
Na mvunja nchiiiiiiiiiiii!!!!!!!
WATU WOTE
Ni huyo huyo Mwananchi.
Watu wanapiga makofi na Vigelegele.
MAMA MKUDE
Jamani tunawaomba sana acheni kulima kando kando
ya mto Mkondoa, acheni kuchungia mifugo yenu kando
ya mto Mkondoa, Jamani hii ni amri ya Serikali, kufanya
hayo yote kuna sababisha mmomonyoko wa
udongo na hatimae husababisha Mafuriko.
MTU 1
(KWA KUROPOKA)
Sasa unataka tulime wapi na kuchungia wapi wakati yale
ndio maeneo yenye rutuba na majani mazuri.
MAMA MKUDE
Nimesema hii ni amri toka Serikalini, na maeneo ya
Kulima na kuchungia yapo mengi sana. Sasa nasema hivi
atakae kwenda kinyume na amri hii akikamatwa Sheria
itachukua mkondo wake, tumetunga sheria ngumu ili
13
tuweze kuulinda mto wetu. Tumechoshwa na mafuriko
katika Wilaya yetu… tukiacha tabia hii iendelee ni sawa
na kulipa dudu liumalo….!!
WATU WOTE
Kidoleeeeeeeeee
MAMA MKUDE
Si ndio jamani………..?
HADHARA
Ndiooooooooo!!!
14
TANGAZO LA TELEVISHENI 2
NDANI : JIONI : NYUMBANI KWA SEKULU
Anaonekana Bwana Sekulu akiwa amekaa na Bwana Mloka na mkewe sebuleni, kwenye
Makochi ya kawaida, ni kajumba kazuri.
SEKULU
Mloka na Shemeji Ahsanteni sana kwa ushauri wenu.
MLOKA
Tunakushauri mengi Sekulu lipi hasa unalotushukuru.?
SEKULU
Hili mliloniambia kwamba kusombewa vitu na mafuriko
sio mwisho wa maisha, nikakakope kamkopo kadogo,
imenisaidia nyumba ndio hii na biashara zangu zinaendelea
vizuri, maana mafuriko ya mto Mkondoa yalinisombea kila
kitu.
MAMA MLOKA
Umeamini sasa Shemeji kukumbwa na mafuriko, sio mwisho
wa maisha.
SEKULU
Ni kweli, Shemeji… Binadamu hutakiwi kukata tama, na mimi
nitawashauri wenzagu wakikutwa na hali kama yangu ya kukumbwa na
mafurio wasikate tamma, maisha yanatakiwa kuendelea…kukatika kwa
koloeo siyo mwisho wa……..
WOTE
Uhunzi……..
15
WILAYA YA MAGHARIBI, UNGUJA- MAFURIKO
TANGAZO LA REDIO 1
WAHUSIKA
:
HABIBA NA SHARIF
MAHALI
:
NYUMBANI KWAO
SAUTI NA MILIO :
MUZIKI KWA MBALI
1. HABIBA
Mimi kuendelea kukaa hapa, unajidangaya, siwezi. Mabondeni
:
utakaa peke yako.
2. SHARIF
:
Mimi ndio baba, tutaendelea kuishi hapa, sipengine.
3. HABIBA
:
Hata kama, wewe ambae unaona kuendelea kukaa hapa ni sawa
endelea, tulipoteza vitu vyetu kibao, wewe mwenyewe kama sio
waokoaji ulikuwa una bebwa na mafuriko, hukomi tu, mimi na
wanangu tutakwenda kukaa huko huko waliko tuhamishia.
4. SHARIF
:
Kwa hiyo tunabishana, si ndiyo? Tutaishi hapa hapa. Kama
kawaida, nimesha weka doti.
5. HABIBA
:
Kuishi mabondeni ni hatari kwetu na familia nzima. Ili kuilinda
familia yako na jamii nzima ni kuhakikisha unaisaidia
kuwashawishi watu wasijenge mabondeni. wewe baki peke yako.
wanangu twendeni…. Twendeni, siwezi kukubali kupoteza maisha
ya familia yangu huku naona….. haya twendeni…….
6. SHARIF
:
Habiba….. wee Habiba…. Rudi hapa.
7. HABIBA
:
Habiba ni jina langu, kwa heri
8. SAUTI NA MILIO :
Mlango unafunguliwa nakufungwa.
16
TANGAZO LA REDIO
2
WAHUSIKA
:
MTENDAJI NA WANANCHI
MAHALI
:
OFISI YA SERIKALI YA MTAA
SAUTI NA MILIO :
KELELE ZA WATU
1. SAUTI NA MILIO:
KELELE ZA WATU HUKU WAKIIMBA
2. MTU 1
(KWA KUPAYUKA ) Kama hataki kuvunja nyumba yake
:
mwenyewe turuhusuni wananchi tuivunje.
3. MTU 2
:
Atajengaje Nyumba yake kwenye mkondo wa mto?
4. MTU 3
:
Kwa nini azibe mifereji ya maji machafu na mto kwa kujenga
jumba lake. Aliondoe haraka.
5. MTU 1
:
Tunataka tumjue ni nani alimpa Kibali cha kujenga kwenye
njia ya mfereji wa maji machafu.
6. MTU 3
:
Avunje yeye mwenyewe kabla hatuja chukua sheria mkononi,
tumechoshwa na mafuriko na maji kujaa ndani ya nyumba zetu
wakati wa mvua.
7. MTU 4
:
Viongozi tunataka maelezo ya kina, kiburi cha kujenga na
kuziba Mfereji na njia ya maji anakitoa wapi?
8. MTENDAJI
:
Tumeona jamani, kweli ni kosa kubwa kujenga na kuziba njia ya
maji, amekubali kuanzia kesho ataanza kuivunja nyumba yake.
9. WOTE
:
WATU WANAPIGA MAKOFI NA KUSHANGILIA
10. MTU 1
:
Asipofanya hivyo kuanzia kesho, tutamuonyesha cha
mtema kuni.
11. SAUTI NA MILIO:
WANASIKIKA WAKIIMBA NYIMBO ZA
KUHAMASISHANA
17
TANGAZO LA TELEVISHENI 1
NDANI : JIONI : KWA BWANA SHARIF : MABONDENI :
Ni ndani nyumbani kwa bwana Sharif, anaonekana amekaa na wanawe wanne, wawili wa kiume
na wawili wa kike, anaonekana mke wa Sharif, Habiba anaonekana amesimama huku anaongea
kwa hasira. Huku akiwa anatoa mabegi na masanduku.
HABIBA
Mimi kuendelea kukaa hapa, unajidangaya, siwezi.
mabondeni utakaa peke yako.
SHARIF
Mimi ndio baba, tutaendelea kuishi hapa, sipengine.
HABIBA
Hata kama, wewe ambae unaona kuendelea kukaa hapa
ni sawa endelea, tulipoteza vitu vyetu Kibao, wewe
mwenyewe kama sio waokoaji ulikuwa Una bebwa na
mafuriko, hukomi tu, mimi na wanangu Tutakwenda kukaa
huko huko waliko tuhamishia.
SHARIF
Kwa hiyo tunabishana, si ndiyo? Tutaishi hapa hapa. Kama
kawaida, nimesha weka doti.
HABIBA
Kuishi mabondeni ni hatari kwetu na familia nzima.
ili kuilinda familia yako na jamii nzima ni kuhakikisha
unaisaidia kuwashawishi watu wasijenge mabondeni.
Wewe baki peke yako. Wanangu twendeni.
Anaonekana akitoka na mizigo huku watoto wakimfuata,
SHARIF
Habiba….. wee Habiba…. Rudi hapa.
HABIBA
Habiba ni jina langu, kwa heri
Mlango unafungwa na kumuacha Sharif amesimama hajui afanye nini.
18
TANGAZO LA TELEVISHENI 2
NJE : MCHANA : MBELE YA OFISI YA SERIKALI YA MTAA (SHEHIA) :
Wanaoneka watu wengi kiasi wakiwa mbele ya Ofisi ya Serikali ya Mtaa (SHEHIA) Wakiwa na
mabango wameyashika mikononi, wengine wameshika wawili wawili, wengine mmoja mmoja
huku wanaimba…mabango yanasomeka hivi.
1. Kama hataki kuvunja nyumba yake mwenyewe turuhusuni wananchi tuivunje.
2. Atajengaje Nyumba yake kwenye mkondo wa mto,
3. Kwa nini azibe mifereji ya maji machafu na mto kwa kujenga jumba lake.
4. Tunataka tumjue ni nani alimpa Kibali cha kujenga kwenye njia ya mfereji wa maji
machafu.
5. Avunje yeye mwenyewe kabla hatuja chukua sheria mkononi, tumechoshwa na mafuriko
na maji kujaa ndani ya nyumba zetu wakati wa mvua.
6. Viongozi tunataka maelezo ya kina, kiburi cha kujenga na kuziba njia ya maji anaitoa
wapi?
MTENDAJI
Tumeona jamani, kweli ni kosa kubwa kujenga na kuziba
njia ya Maji, amekubali kuanzia kesho ataanza kuivunja
nyumba yake.
Watu wanapiga makofi na kushangilia
MTU 1
Asipofanya hivyo kuanzia kesho, tutamuonyesha cha
mtema kuni.
Wanatawanyika huku wanaimba kwa furaha.
19
WILAYA YA LONGIDO, ARUSHA – UKAME
TANGAZO LA REDIO
1
WAHUSIKA
:
OLE MUDIKI NA MOLLEL
MAHALI
:
KWA MOLLLEL
SAUTI NA MILIO :
MILIO YA NGOMBE NA MBUZI
1. O’MUDIKI
:
Nasema hivi, nataka mifugo yangu isssei, utaniusi.
2. MOLLEL
:
Mfugo hata mmoja sikupi, nenda shambani kwangu kaangalie
walivyo nitenda,
3. O’ MUDIKI
:
Hayo mimi sijui ninachotaka nataka munyama yangu la sivyo
nitachukua kwa ngufu.
4. MOLLEL
:
(KWA HASIRA) Jaribu nikuonyese, unaleta utani kwa mali
yangu , kila siku tunaambiwa, fuga wanyama wachache wenye tija,
ni hivi tunatakiwa kufuga kisanyansi, unaporuhusu ng’ombe na
mbusi wanatembea tembea tena wengi, huichakaza Ardhi yenye
rutuba na kusababisha Jangwa na ukame.
5. O’MUDIKI
:
Mimi hayo sijui nataka munyama yangu
6. MOLLEL
:
Kuchunga hovyo ni makosa, Ng’ombe wote hao wa nini?Ng’ombe
alfu mbili wa nini wote hao, wakipita mahali kwenda machungani,
wanasababisha mmomonyoko wa udongo ambao huleta ukame,
acha kuchunga hivyo mifugo yako, umesikia?
7. O’MUDIKI
:
Nimesikia mzee wangu, ...sasa nitapata mufugo yangu au sipati?
20
TANGAZO LA REDIO 2
WAHUSIKA
:
EDWARD, OLE MOLOIMETT NA MA’MOLOIMENT
MAHALI
:
SHAMBANI KWA MOLOIMETT
SAUTI NA MILIO :
SAUTI ZA NDEGE
1. EDWARD
Bwana Moloimett naona unapanda miti, huoni ni kama
:
unapotesa muda wako tu.
2. MOLOIMETT :
Kwa nini nasema hivyo? Huoni kama ukame nasidi
3. EDWARD
Sasa kwani ukame nasababishwa na miti, hii ni laana.
:
Lazima tuchinje munyama tutoe kafara.
4. MOLOIMETT :
Huko ni kujidanganya, laana hiyo tumeitafuta sisi wenyewe
kwa kukata miti, la muhimu ni sisi wote kama jamii nzima
kuhakikisha tunapanda miti kama vile hatuna akili nzuri, na
hili ni jukumu langu mimi, wewe, yule na wana Longido
wote.
5. MA’MOLOIMETT:
Hilo ndilo tunalotakiwa kufanya, tuhamasishane
kuhakikisha tunapanda miti tuondokane na hili Janga la
ukame,…, hali inatisha.
6. EDWARD
:
Ni kweli hata mimi taungana na nyinyi katika hilo hali
natisha, jua nawaka kama moto ya jehanamu
21
TANGAZO LA TELEVISHENI 1
NJE
: JIONI : KWA MOLLEL : NJE YA NYUMBA :
Anaonekana Mollel akiwa anaongea na Ole Mudiki, Ole Mudiki anaonekana kuongea kwa
hasira
OLE MUDIKI
Nasema hivi, nataka mifugo yangu isssei, utaniusi.
MOLLEL
Mfugo hata mmoja sikupi, nenda shambani kwangu
kaangalie walivyo nitenda,
OLE MUDIKI
Hayo mimi sijui ninachotaka nataka munyama yangu
la sivyo nitachukua kwa ngufu.
MOLLEL
(KWA HASIRA)
Jaribu nikuonyese, unaleta utani kwa mali yangu,kila siku
tunaambiwa, fuga wanyama wachache wenye tija, ni hivi
tunatakiwa kufuga kisanyansi, unaporuhusu ng’ombe
na Mbusi wanatembea tembea tena wengi, huichakaza
Ardhi yenye rutuba na kusababisha Jangwa na ukame.
OLE MUDIKI
Mimi hayo sijui nataka munyama yangu
MOLLEL
Kuchunga hovyo ni makosa, Ng’ombe wote hao wa nini?
Ng’ombe alfu mbili wa nini wote hao, wakipita mahali
kwenda machungani, wanasababisha mmomonyoko wa
udongo ambao huleta ukame, acha kuchunga hivyo
mifugo yako, umesikia?
OLE MUDIKI
Nimesikia mzee wangu, …….sasa nitapata mufugo yangu
au sipati?
22
TANGAZO LA TELEVISHENI 2
NJE : ASUBUHI : SHAMBANI : KIJIJINI :
Anaonekana Bwana Ole Moloimett akiwa na Mkewe Martha wakiwa wanapanda Miti, kando
yao anaoneka Bwana Edward akiwa anapita anasimama na kuwaangalia.
EDWARD
Bwana Moloimett naona unapanda miti, huoni ni
kama unapotesa muda wako tu.
MOLOIMETT
Kwa nini nasema hivyo? Huoni kama ukame nasidi
EDWARD
Sasa kwani ukame nasababishwa na miti, hii ni laana.
lazima tuchinje munyama tutoe kafara.
MOLOIMETT
Huko ni kujidanganya, laana hiyo tumeitafuta sisi
wenyewe kwa kukata miti, la muhimu ni sisi wote
kama jamii nzima kuhakikisha tunapanda miti kama
vile hatuna akili nzuri, na hili ni jukumu langu mimi,
wewe, yule na wana Longido wote.
MAMA MOLOIMETT
Hilo ndilo tunalotakiwa kufanya, tuhamasishane
kuhakikisha tunapanda miti tuondokani na hili
janga la ukame, hali inatisha.
EDWARD
Ni kweli hata mimi taungana na nyinyi katika hilo
hali natisha, jua nawaka kama moto ya jehanamu
23
WILAYA YA KINONDONI, DAR ES SALAAM-MAFURIKO
TANGAZO LA REDIO 1
WAHUSIKA
:
KAKA, MGAMBO, DADA1, DADA 2 NA MWENYEKITI
MAHALI
:
MTAANI
SAUTI NA MILIO :
HONI NA NGURUMO ZA MAGARI
1. DADA 1
Mwenzangu wee tupa haraka hizo takataka zako, nasikia
:
wakikukamata …… heeeeee
2. DADA 2
:
Achaaaaa wewe
3. KIJANA
:
Wanazuga tu
4. MGAMBO
:
Hatuzugi tuko makini, kwa hiyo mko chini ya ulinzi, wachafuzi
wakubwa wa Mazingira… simama hapo.
5. DADA 1
:
Kosa letu ni lipi? mlitaka tukatupie wapi takataka?
6. M’KITI
:
Nyumbani kwako unajiwekea pipa, unajaza uchafu ukisubiri
magari ya kusomba taka ya pite. Hapa umetupa kwenye mfereji
tena ndani ya mfereji.
Wakati wa mvua ndio hu sababisha
mafuriko. Na huu ni uchafunzi mbaya sana wa…………..
7. DADA 2
:
(Akiingilia) Lakini sio sisi peke yetu, mtaa wote huu tunatupa
Takataka hapa.
8. MGAMBO
:
Aliyeshikwa na Ngozi ndio Mwizi wa Ng’ombe, twende. Sheria
ikachukue nafasi yake…….
9. M’KITI
:
Dawa ya watu kama hawa ni kuwakamata na kuwapeleka
mahakamani, hali kama hii haikubaliki, mafuriko yaliyo pita watu
wengi walipoteza
maisha na mali zao, kwa ujinga huu
huu…….Nasema uongo jamani…….?
24
TANGAZO LA REDIO 2
WAHUSIKA
:
HAMADI NA MWAKITUTA
MAHALI
:
NJIANI
SAUTI NA MILIO :
SAUTI ZA NDEGE
1. HAMADI
:
Karibu ndugu yangu….. Mwakituta karibu.
2. M’TUTA
:
Hamadi ndugu yangu si tulihamishwa huku mabondeni
yaani na nyumba ndio umeamua kuijenga vizuri zaidi.
3. HAMADI
:
Siwezi mimi kuhama hapa nikaishi porini kule, mambo
yote mjini, liwalo na liwe.
4. M’TUTA
:
Hayo sio maneno, hapa unaiweka familia yako na wewe
mwenyewe kwenye hatari kubwa, mafuriko yakija hapa
nani atapona, haya maeneo ya mabondeni hayafai jamani.
Hamadi umesahau uliponea tundu la Sindano,….. umesahau
ee, ama kweli sikio la kufa….. halisikii dawa
5. HAMADI
:
Bwana wewe yaliyopita si ndwele………
6. M’TUTA
:
Tugange kifo chako na familia yako kwa kusombwa na mafuriko.
Si ndio…… jamani tuambiwe mara ngapi maeneo ya mabondeni
ni hatari kuishi, hayafai…… hapa ni kifo mkononi…..
7. HAMADI
:
Najua lakini sasa mimi nifanyeje na huku ndio biashara
zangu ziliko, nifanyeje……. Mwakituta?
25
TANGAZO LA TELEVISHENI 1
NDANI : MTAANI : JIONI : USWAHILINI :
Unaonekana mfereji wa maji machafu ukiwa umejaa uchafu mpaka juu, unaonekana kabisa
kwamba maji yakija hayataweza kupita, yanaonekana maeneo zaidi yaliyo jaa uchafu mpaka
kuziba njia za kupitia maji. Wanaonekana akina dada wawili na Kijana mmoja wakija wakiwa na
viroba vilivyo jaa uchafu na kutupa kwenye mfereji ule ule, wakati wanamalizia kutupa tu
wanaonekana Mgambo kama watatu na watu wengine wawili wakiwa wamevaa kiraia,
wanawakamata wale wanawake na yule kijana,
MGAMBO 1
Mko chini ya ulinzi, wachafuzi wakubwa wa Mazingira
DADA 1
Kosa letu ni lipi? Mlitaka tukatupie wapi takataka?
MWENYEKITI
Nyumbani kwako unajiwekea pipa, unajaza uchafu
ukisubiri magari ya kusomba taka ya pite. Hapa
mnapotupa hivi wakati wa mvua ndio kuna sababisha
mafuriko. Na huu ni uchafunzi mbaya sana wa mazingira
DADA 2
Lakini sio sisi peke yetu, mtaa wote huu tunatupa
takataka hapa.
MGAMBO 1
Aliyeshikwa na ngozi ndio mwizi wa Ng’ombe, twende.
sheria ikachukue nafasi yake…….
MWENYEKITI
Dawa ya watu kama hawa ni kuwakamata na kuwapeleka
mahakamani, hali kama hii haikubaliki, mafuriko yaliyo
pita watu wengi walipoteza maisha na mali zao, kwa ujinga huu huu.
Nasema uongo jamani…….?
Anageuka kuwaangalia wenzie na watuhumiwa wao, wanaonekana wanamuangalia na
kukubaliana nae, Kisha anageukia Kamera.
26
TANGAZO LA TELEVISHENI 2
NDANI : JIONI : MBELE YA NYUMBA : MTAANI : USWAHILINI :
Anaonekana Bwana Hamadi na Bwana Mwakituta wakiwa wanatembea kwenye maeneo ya
Mabondeni, zinaonekana nyumba zikiwa zimejengwa kwenye Bonde, wanafika mbele ya
nyumba moja na yenyewe iko Bondeni.
HAMADI
Karibu ndugu yangu….. Mwakituta karibu.
MWAKITUTA
(ANAONEKANA AKIANGALIA HUKU NA KULE)
Hamadi ndugu yangu si tulihamishwa huku mabondeni
yaani na nyumba ndio umeijenga vizuri zaidi.
HAMADI
Siwezi mimi kuhama hapa nikaishi porini kule, mambo
yote mjini, liwalo na liwe.
MWAKITUTA
Hayo sio maneno, hapa unaiweka familia yako na wewe
mwenyewe kwenye hatari kubwa, mafuriko yakija hapa
nani atapona, haya maeneo ya mabondeni hayafai jamani.
Hamadi umesahau uliponea tundu la Sindano, umesahau ee !
HAMADI
Bwana wewe yaliyopita si ndwele………
MWAKITUTA
Tugange kifo chako na familia yako kwa kusombwa na
mafuriko. Si ndio…… jamani tuambiwe mara ngapi
maeneo ya mabondeni ni hatari kuishi, hayafai.
HAMADI
Najua lakini sasa mimi nifanyeje na huku ndio biashara
zangu ziliko, nifanyeje…..
27
WILAYA YA HANDENI, TANGA-MLIPUKO WA KIPINDUPINDU
Ujumbe: Kuripoti mapema milipuko ya kipindupindu, dalili zake na matibabu ya mapema
pamoja na kumpa mgonjwa mchanganyiko wa maji, chumvi na sukuri (ORS) husaidia kuokoa
maisha.
MCHORO NAMBA 1
28
Ujumbe: Jilinde mwenyewe, familia yako na jamii yako ili kuepuka maambukizi ya
kipindupindu kwa kuchemsha maji ya kunywa
MCHORO NAMBA 2
29
Ujumbe: Wakinge uwapendao kwa kutunza mazingira yako: uchafu hueneza kipindupindu.
MCHORO NAMBA 3
30
Ujumbe: Kipindupindu kinauwa: njia salama ya kujilinda wewe na familia yako ni kuepuka
kunywa na kula vyakula vya barabarani vya baridi.
MCHORO NAMBA 4
31
WILAYA YA KILOSA, MOROGORO-MAFURIKO
Ujumbe: Mafuriko yanauwa, mara upatapo taarifa ya kuondoka kwenye eneo hatarishi ondoka
haraka ili uokoe maisha yako na familia yako.
MCHORO NAMBA 1
32
Ujumbe: Mafuriko yanaua; jilinde mwenyewe, familia yako na jamii yako kwa ujumla kwa
kutunza kingo za mto Mkondoa.
MCHORO NAMBA 2
33
Ujumbe: Ikinge jamii na familia yako na hatari ya mafuriko kwa kupanda miti kandokando ya
mto Mkondoa.
MCHORO NAMBA 3
34
Ujumbe: Upatikanaji wa mikopo midogo midogo husaidia kujenga nyumba zilizoharibiwa na
mafuriko na kuendeleza biashara ndogondogo.
MCHORO NAMBA 4
35
WILAYA YA MICHEWENI, PEMBA-UKAME
Ujumbe: wanaume na wanawake wote kwa pamoja tujiunge kwenye shughuli za kilimo ili
tuongeze upatikanaji wa chakula katika familia zetu.
MCHORO NAMBA 1
36
Ujumbe: Vuna maji ya mvua na anzisha kilimo cha umwagiliaji ili kuongeza kipato na kuondoa
njaa katika familia yako
MCHORO NAMBA 2
37
Ujumbe: Ikinge jamii na familia yako dhidi ya ukame kwa kupanda miti
MCHORO NAMBA 3
38
Ujumbe: Panda mazao yanayostahimili ukame ili kupambana na upungufu wa chakula
MCHORO NAMBA 4
39
WILAYA YA KINONDONI, DAR ES SALAAM-MAFURIKO
Ujumbe: Maeneo yanayokumbwa na mafuriko mara kwa mara ni hatari, jikinge wewe na
familia yako, usijenge na kuishi maeneo hayo
MCHORO NAMBA 1
40
Ujumbe: Jikinge wewe na familia yako, usijenge na kuishi kwenye mkondo wa maji
MCHORO NAMBA 2
41
Ujumbe: Ikinge jamii yako na mafuriko; usichimbe mchanga katika mto Msimbazi
MCHORO NAMBA 3
42
Ujumba: Weka mazingira yako safi usitupe taka katika mifereji; kuepuka mafuriko
MCHORO NAMBA 4
43
WILAYA YA LONGIDO, ARUSHA-UKAME
Ujumbe: Punguza namba ya mifugo kwenye kaya yako kuepuka uharibifu wa mazingira
MCHORO NAMBA 1
44
Ujumbe: Ili kupunguza uhaba wa chakula kwenye familia yako, panda mazao yanayostahimili
ukame
MCHORO NAMBA 2
45
Ujumbe: Kufuga mifugo mingi kunasababisha uharibifu wa mazingira; tunza mazingira kwa
kupunguza idadi ya mifugo
MCHORO NAMBA 3
46
Ujumbe: Ikinge jamii yako dhidi ya ukame kwa kupanda miti
MCHORO NAMBA 4
47
WILAYA YA MAGHARIBI, UNGUJA-MAFURIKO
Uumbe: Ikinge familia yako dhidi ya mafuriko, usizibe mifereji ya asili kwa kujenga nyumba
kwenye maeneo hayo
MCHORO NAMBA 1
48
Ujumbe: Maeneo yanayokumbwa na mafuriko mara kwa mara ni hatari, jikinge wewe na
familia yako, usijenge na kuishi maeneo hayo
MCHORO NAMBA 2
49
Ujumbe: Weka mazingira yako safi; usitupe taka katika mifereji ya maji ya mvua
MCHORO NAMBA 3
50
KIAMBATANISHO No 1: UJUMBE MHIMU NA NJIA ZA MAWASILIANO ZINAZOTUMIKA KWA SASA NA NJIA
MPYA ZILIZOPENDEKEZWA KUTUMIKA
Wilaya
Handeni
Ujumbe
Njia za mawasiliano
Televisheni
Kuchemsha maji ya
kunywa ni moja ya
njia bora za kuikinga
familia yako kutokana
na maambukizi ya
ugonjwa wa
kipindupindu
Wakinge uwapendao:
uchafu hueneza
ugonjwa wa
kipindupindu, weka
mazingira yako katika
hali ya usafi
Kuripoti mapema
dalili za ugonjwa wa
kipindupindu pamoja
na matibabu ya
mapema na kumpatia
mgonjwa
mchanganyiko wa
maji, chumvi na sukuri
(ORS) huokoa maisha
Hii ni dharura: njia
sahihi ya kujilinda
wewe na familia yako
na ugonjwa wa
kipindupindu ni
kuepuka misongamano
isiyo ya lazima pamoja
na kutokunywa na
kula vyakula vya
baridi vya barabarani
Jikinge wewe
mwenyewe pamoja na
Kipaza
Sauti
Magazeti
Broshua
Posita
Mbao za
matanga
zo


































Redio

DVD


51



Mabango

Simu za
mkononi

Mtandao
wa
Intaneti
Uso
Kwa
Uso

Mawasi
liano ya
kijadi

familia yako na
ugonjwa wa
kipindupindu kwa
kunawa mikono na
maji ya moto na
sabuni kabla ya kula
na baada ya kutoka
chooni
Tumia choo siku zote
uepuke kueneza
ugonjwa wa
kipindupindu
Jikinge wewe, familia
yako na jamii yako
kwa ujumla kutokana
na maambukizi ya
ugonjwa wa kipindu
pindu: chemsha maji
ya kunywa kila siku
Michewen
i
Ilinde jamii yako na
familia yako kutokana
na athari za janga la
ukame kwa kupanda
miti
Ikinge jamii yako na
uharibifu wa
mazingira: usifanye
shughuli za kuchimba
mchanga na
kutengeneza tofali za
mawe
Epuka uchimbaji wa
mchanga pamoja na
utengenezaji wa tofali
za mawe ili kupunguza
athari za uharibifu wa
mazingira

































































52

Kinondoni
Wanaume na
wanawake sote kwa
pamoja
tujishughulishe na
kilimo ili kuongeza
upatikanaji wa chakula
katika familia zetu
Panda mazao
yanayostahimili
ukame ili kukabiliana
na madhara
yatokanayo na ukame
kama vile upungufu
wa chakula
Jishughulishe na
kilimo ili kupunguza
tatizo la njaa na
kuondoa utapiamlo
katika familia yako
Vuna maji ya mvua na
kujishughilisha na
kilimo cha umwagiliaji
ili kuongeza
upatikanaji wa chakula
na kuondoa njaa katika
familia yako












































Maeneo ya mabondeni
ni hatari sana kwa
mafuriko: ilinde
familia yako na wewe
mwenyewe usijenge
nyumba na kuishi
katika maeneo hayo
Ilinde jamii yako na
janga la mafuriko:
Usichimbe mchanga
kando kando ya mto
msimbazi
Iweke jamii yako
katika hali ya



































53



usafi,usitupe taka
ngumu kwenye
mifereji ya maji ya
mvua
Kilosa
Mafuriko yanaua:
mara usikiapo
tahadhari ya mafuriko
ikitolewa, ondoka
haraka sana eneo
hatarishi na uende
eneo salama
Tafuta mikopo midogo
mdogo ili ikusaidie
kukarabati nyumba
yako na biashara yako
iliyo athirika na
mafuriko, kuna maisha
hata baada ya
mafuriko
Ilinde jamii yako na
familia yako kutokana
na mafuriko kwa
kupanda miti na
matete kando kando ya
mto mkondoa
Kuchungia kando
kando ya mto
Mkondoa
kunasababisha
mmomonyoko wa
udongo na kupungaza
kina cha mto na
hatimaye kusababisha
mafuriko:Ilinde jamii
yako kwa kuacha
kuchungia mifugo
kando kando ya mto
Mkondoa
Mafuriko yanaua:
usilime kando ya mto
Mkondoa kwani
shghuli za kilimo


































































54
zinachangia kuongeza
hatari ya kutokea kwa
mafuriko
Mafuriko yanaua:
mara upatapo
tahadhari ya mafuriko,
tafadhari ondoka
haraka sana eneo
hatarishi na uende
eneo salama
Jitahidi upate mikopo
midogo midogo ili
uweze kukarabati
nymba yako na
biashara yako
iliyoathirika na
mafuriko: Kuna
maisha hata baada ya
mafuriko
Jilinde wewe na
familia yako na jamii
yako kwa ujumla
kutokana na mafuriko
kwa kulinda tuta na
kingo za mto
Mkondoa
Magharibi
Maeneo ya mabondeni
ni hatari sana kwa
mafuriko, jilinde
wewe na familia yako:
usiishi na kujenga
katika maeneo hayo
Ilinde jamii yako na
mafuriko: usizibe
mifereji ya asili ya
maji kwa kujenga
nyumba katika maeneo
hayo
Iweke jamii yako
katika hali ya usafi:
usitupe taka ngumu














































































55
katika mifereji ya maji
ya mvua
Mafuriko yanaua:
mara upatapo
tahadhari ya mafuriko
ondoka haraka sana
eneo hatarishi na
uende eneo salama
Jitahidi upate mikopo
midogo midogo ili
uweze kukarabati
nymba yako na
biashara yako iliyo
athirika na mafuriko;
Kuna maisha hata
baada ya mafuriko
Uchungaji holela wa
mifugo unasababisha
uharibifu wa
mazingira: ilinde jamii
yako kwa kufuga
kisasa na kuacha
kuchunga mifungo
hovyo
Fuga kisasa kwa
kupunguza idadi ya
mifungo yako ili
kupunguza athari za
uharibifu wa
mazingira




















































Ili kuongeza


 







upatikanaji wa
chakula katika
familia yako panda
mazao
yanayostahimili
ukame
Ilinde jamii yako na 

 







athari za ukame kwa
kupanda miti
Angalizo: Rangi nyeusi inaonyesha njia zilizopo za mawasiliano na rangi nyekudu inaonyesha njia mpya za mawasiliano zilizo pendekezwa




Longido
56