NORTH EASTERN DIOCESE

Transcription

NORTH EASTERN DIOCESE
NORTH EASTERN DIOCESE
EVANGELICAL LUTHERAN CHURCH IN TANZANIA
CLINICAL OFFICERS TRANING CENTRE BUMBULI
Tel: +255-27-2640360
Tel:+255-27-2640360
Fax: +255-27-2640360
P.O.Box 9,
Bumbuli, Tanzania.
Email:[email protected]
Kumb Na: COTC/BK/1/____________
01ST /08/2014
_________________________________________
_________________________________________
_________________________________________
Yah: MAFUNZO YA KUJIENDELEZA KWA MWAKA WA MASOMO 2014/2015
Napenda kukuarifu kuwa umechaguliwa kujiunga na mafunzo ya Clinical Officer katika
chuo hiki. Mafunzo yaha ni ya miaka miwili.
Mafunzo yaataanza tarehe 6th, Oktoba, 2014. Unatakiwa ufike chuoni siku mbili kabla ya
masomo kuanza. Napenda ieleweke kwamba nafasi yako itahesabika kupotea kabisa na
kujazwa na mtu mwingine endapo hautafika katika kipindi kilichotajwa.
Gharama za mafunzo, unatakiwa kulipa ada kiasi cha shilingi (TZS.1, 900,400.00) kwa
mwaka. Unaweza kulipa gharama hii kwa awamu moja au mbili. Malipo yote ya Ada ni
kupitia Benki katika akaunti ya chuo, NMB Lushoto, ELCT NED CLINICAL OFFICERS
TRAINING CENTRE A/C.No: 4161300005.
Kabla ya kwenda choni hakikisha afya yako imepimwa na kupata cheti (medical certificate)
kutoka kwa Daktari., Cheti hicho itakubidi ukikabidhi kwa Mkuu wa Chuo mara tu ufikapo
chuoni.
Wakati wote utakapokuwa chuoni unatakiwa kutii sheria za nchi na za chuo. Vilevile
ieleweke kwamba masuala yote ya mwanfunzi anapokuwa chuoni yatashuhulikiwa na
Uongozi wa chuo, endapo itakuwepo lazima ya suala la mwanafunzi kughulikiwa na Wizara
makao makuu, basi maombi au matatizo yote yapitie kwa Mkuu wa Chuo kabla ya
kuwasilishwa.
Utaratibu wa matibabu yote yatagharamiwa na mwanafunzi mwenyewe kupitia bima ya
taifa ya afya.
Page 1 of 3
Usafiri wa kwenda na kurudi chuoni ni gharama ya mwanafunzi na wala si jukumu la Chuo.
Hakikisha unakuwa na fedha za kutosha kwa asjili ya mwatumizi yako madogo madogo
kwa kipindi utakapokuwa chuoni.
Kila mwanafunzi anatakiwa kufika chuoni na vifaa vifuatavyo:SARE ZA CHUO:
 Mwanamke: Magauni mawili (2) meupe ya mikono mifupi, viatu vyeupe, vyeusi au
kahawia vyenye visigino vifupi.

Mwanaume: Suruali mbili (2) za rangi ya khaki na mashati mawili rangi nyeupe ya
mikono mifupi. Viatu vya ngozi nyeusi au kahawia.
UNATAKIWA KUJA NA MAHITAJI YAFUTAYO:
1. Nguo za michezo mbalimbali
2. Ndoo ya maji aina ya “Plastic”
3. Picha nne(4) Passport size kwa ajili ya kumbukumbu.
4. Cheti halisi cha cha kuhitimu kidato cha nne
5. Vitabu katika kozi husika inapowezekana.
6. Vifaa vya kuandikia kwa mfano madaftari, kalamu, rula n.k.
7. Mwamvuli au koti la mvua.
8. Viatu aina ya Buti za mvua
9. Shuka - 4, mto -, blanketi -1, chandarua -1, taulo na foronya
MWONGOZO WA GHARAMA/AINISHO LA ADA
S/R
ITEM
1
TUITION FEES
2
GHARAMA YA MITIHANI WA KUHITIMU
3
IDENTITY CARD
4
PRACTICAL PROCEDURE BOOK
5
PRACITICUM GUIDE BOOK
6
HEALTH INSURANCE
7
SPORTS
8
CAUTION MONEY
9
NACTE STUDENT REGISTRATION FEES
10
APPLICATION FORM
TOTAL AMOUNT
COST
1,550,000.00
150,000.00
5,000.00
50,000.00
30,000.00
50,400.00
10,000.00
10,000.00
15,000.00
30,000.00
1,900,400.00
Page 2 of 3
2
MAHALI PA KUISHI MWANAFUNZI






3
Kila mwanafunzi atagharamia mahali pa kuishi kipindi chote atakapokuwa chuoni.
Gharama kwa mwezi ni shilingi hamsini elfu tu (TZS.50, 000.00).
Kwa muhula ni shilingi laki mbili hamsini elfu tu (TZS.250,000.00)
Hivyo basi gharama kwa miezi kumi mwanafunzi atakapokuwa chuono ni
shilingi Laki tano tu (TZS.500, 000.00).
Fedha hizo zitalipwa katika akaunti ya chuo.
Fedha hizo zaweza kulipwa kwa mara moja au awamu mbili kupitia
akaunti ya chuo kama ilivyoelekezwa katika ukurasa wa kwanza.
CHAKULA CHA KILA SIKU
Kila mwanafunzi atagharamia chakula chake kwa kununua katika mgahawa wa chuo
kwa fedha tasilim.
MAELEKEZO KUHUSU MAHALI CHUO KILIPO




Chuo kinapatikana Bumbuli katika halmashauri ya Bumbuli wilaya ya
Lushoto.
Ukiwa Dar es Salaam pakia Basi la Bumbuli
Ukiwa Arusha/Moshi/Tanga pakia basi la Bumbuli
Au pakia basi hadi Mombo au Soni halafu panda mabasi ya kuelekea
Bumbuli
Nakutakia kila kheri katika mafunzo yako
Dr. Ronald Erasto Msangi
MKUU WA CHUO
Page 3 of 3